• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

CCM yawataka Watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo

Posted on: April 24th, 2025

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi leo ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Mara katika Wilaya ya Butiama na kuwataka watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.

Akizungumza katika ziara ya miaka 61 ya Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar katika Wilaya ya Butiama, Dkt. Nchimbi amesema katika uhai wake Baba wa Taifa alihamasisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa na kukemea ubaguzi wa aina yoyote ile.

“Baba wa Taifa alipigania sana amani, umoja na mshikamano wa Tanzania na akaeneza lugha ya Kishwahili kwa Watanzania wote ili kuujenga umoja wa Kitaifa, tuendelee kumuenzi kwa vitendo kwa kuunga mkono mazuri yote aliyotuachia” amesema Mhe. Nchimbi.  

Balozi Nchimbi amewataka Watanzania kujihadhari na viongozi wa siasa wanaohamasisha uvunjifu wa amani, ukabila na vurugu na badala yake kutumia uchaguzi unaokuja kuwachagua viongozi bora wanaopenda maendeleo.  

Mhe. Nchimbi amesema miradi aliyoitembelea katika Mkoa wa Mara ya Uwanja wa Ndege Musoma, Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Chuo Kikuu cha MJNUAT Butiama ni miradi ya kimkakati na inaenzi maono na matamanio ya Mwalimu Nyerere na Serikali ya awamu ya sita imeitekeleza kwa ufanisi mkubwa.

Mhe. Nchimbi amewataka wanachama wa CCM na wananchi wa Wilaya ya Butiama kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, kuhuisha taarifa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuhakikisha kuwa kura za CCM ni asilimia 100 ili kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amesema ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati katika Wilaya ya Butiama imebadilisha sura ya Butiama kimaendeleo.

Mhe. Sagini ameitaja miradi hiyo kuwa ni Chuo Kikuu cha MJNUAT Butiama, Sekondari ya Amali ya Mkoa wa Mara, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na Chuo cha VETA, mradi wa maji wa Mgango- Kiabakari- Butiama ambayo imelifanya eneo hilo kuwa eneo na hali tofauti kuliko lilivyokuwa awali.

Mhe. Sagini amemuomba Mhe. Nchimbi kuingiza mradi wa ukarabati wa Daraja la Kirumi lililopo katika Mto Mara katika Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2025-2030 ili daraja hilo liwekwe katika miradi ya kipaumbele katika utekelezaji wa ilani hiyo.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nchimbi ametembelea Kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ametembelea na kukagua ukarabati na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) Butiama na kuzungumza na wananchi katika Kampasi kuu ya chuo hicho na kuwasalimia wananchi katika eneo la Kiabakari.

Balozi Nchimbi ameambatana na viongozi na Watendaji wa CCM na Serikali na kauli mbiu ya miaka 61 ya Muungano ni “Muungano wetu ni Dhamana, heshima na tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”. 

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.