• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Units
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

Posted on: June 18th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Dkt. Khalfan Haule amewataka wadau wa zao la tumbaku kuzingatia miongozo na kanuni za kilimo cha zao la tumbaku ili kuongeza uzalishaji na kuboresha hali ya wakulima wa zao hilo.

Mhe. Haule ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano wa kwanza wa wadau wa zao la tumbaku uliowaleta pamoja wakulima, wanunuzi, wawakilishi wa Serikali na taasisi za kifedha katika Mkoa wa Mara uliofanyika tarehe 17 Juni, 2025 katika Hoteli ya Kisare iliyopo katika Mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti.

“Mafanikio katika kilimo cha tumbaku yanategemea sana kufuatwa kwa taratibu za ulimaji na uvunaji wa zao hilo ili kuleta manufaa makubwa kwa mkulima kama inavyokusudiwa, bila hivyo wakulima watakuwa wanahangaika tu bila mafanikio” amesema Dkt. Haule.

Dkt. Haule amesema kwa kuzingatia kanuni na miongozo itawasaidia wakulima kuepusha hasara, kupunguza magonjwa ya mimea na kuongeza mavuno kwa ekari, jambo ambalo litawawezesha wakulima kunufaika zaidi na jasho lao.

Dkt. Haule amesema Serikali imetenga fedha nyingi kwa ajili ya ruzuku katika zao la tumbaku hivyo amewasisitiza wadau wote kusimamia miongozo ya kitaalamu ya kilimo cha tumbaku kuanzia kupanda, utunzaji, uvunaji, ukusanyaji wa tumbaku ili kupata tumbaku bora inayokidhi viwango vya ndani na nje ya nchi.

Lengo la mkutano huo wa wadau ni kuboresha uzalishaji wa tumbaku, kuboresha upatikanaji wa masoko na ustawi wa wakulima wa zao hilo na kutafuta suluhu ya changamato zinazoikabili kilimo cha tumbaku katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Haule ametumia fursa hiyo kukemea tabia ya utoroshaji wa tumbaku kuelekea nchi jirani na kuwatahadhalisha wadau hao kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kutorosha tubaku katika Mkoa wa Mara. 

Aidha, Dkt. Haule amewataka wanunuzi wa tumbaku na taasisi zinazotoa pembejeo kutoa elimu sahihi na endelevu kwa wakulima wa zao la tumbaku ili wakulima waweze kufaidika na kilimo cha tumbaku na kuendeleza uchumi wao binafsi na Taifa lao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakulima wa Mara Cooperative Union (WAMACU) LTD Bwana Momanyi Range ameomba ushirikiano baina ya Serikali, wakulima na wataalam ili zao la tumbaku liweze kuwa na tija kwa pande zote.

Bwana Range amesema kwa sasa wakulima wameitikia kulima tumbaku na hususan katika Wilaya ya Serengeti na kuwaomba wadau kuendelea kutoa elimu ili wakulima waweze kuboresha uzalishaji wa tumbaku na wananchi wengi zaidi waweze kulima tumbaku katika Mkoa wa Mara.

Announcements

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru Wapitisha miradi 68 ya bilioni 26.5 Mara

    August 23, 2025
  • RC Mtambi akutana na viongozi wa dini na kuwasistiza kuhamasisha amani

    August 22, 2025
  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.