Mkoa wa Mara umekuwa mshindi wa pili katika mashindano ya 29 ya Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) Taifa kwa mwaka 2025 yaliyokuwa yanafanyika katika Manispaa ya Iringa na kuhitimishwa leo.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeonyesha kuwa Mkoa wa Mara umepata jumla ya alama 173 na kushika nafasi ya pili katika mashindnao hayo.
Katika mashindano hayo, Mkoa wa Mara umefanya vizuri katika michezo ya handball (wasichana), soka (wasichana), riadha (wavulana) na (wasichana) na usafi kwa (wavulana) ambapo imepata alama 20 katika kila kipengele.
Kwa matokeo hayo Mkoa wa Mara umepanda kwa nafasi moja katika mashindano yam waka huu baada ya mwaka 2024 kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya 28 ya UMITASHUMTA kitaifa.
Taarifa ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeonyesha kuwa Mkoa wa Mwanza umeongoza kitaifa kwa kupata alama 230 wakati Mkoa wa Tabora ukishika nafasi ya tatu Kitaifa baada ya kupata alama 151.
Mashindano hayo yalifunguliwa Rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 6 Juni, 2025 yameahirishwa rasmi leo tarehe 18 Juni, 2025 kupisha mashindnao ya Umoja wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) yanayoanza rasmi tarehe 19 Juni, 2025 katika Manispaa ya Iringa.
Mashindano hayo yaliihusisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Mikoa iliyofanya vibaya ni pamoja na Tanga ambayo imepata alama 80 na kushika nafasi ya 24, Ruvuma alama 75 na kushika nafasi ya 25 na Lindi alama 71.8 na kushika nafasi ya 26.
Sekretarieti ya Mkoa wa Mara inaitakia kila la Kheri timu ya Mkoa wa Mara inayoshiriki michezo ya Umoja wa Shule za Sekondari (UMISETA).
Katibu Tawala Mkoa wa Mara
Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara
Telephone: +255282622305
Mobile:
Email: ras.mara@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.