• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Waziri wa Madini apiga marufuku uchimbaji usiku

Posted on: June 15th, 2020

Waziri wa Madini Mheshimiwa Dotto Biteko amepiga marufuku uchimbaji wa madini usiku kwa wachimbaji wadogo katika Mgodi wa Irasanilo uliopo katika eneo la Buhemba katika Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Biteko ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Juni 2020 wakati alipokuwa anazungumza na wachimbaji na wananchi wa eneo la Buhemba kufuatia ajali iliyotokea katika eneo hilo na kuua wachimbaji wawili na wengine nane kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo.

“Kuanzia sasa shughuli zote za uchimbaji katika eneo hili zifanyike mchana ni marufuku kufanyika usiku” alisema Biteko. Aidha amemtaka mwajiri wa wachimbaji waliofariki na waliojeruhiwa katika ajali hiyo kulipa fidia, kugharamia matibabu, mazishi na msiba kwa mujibu wa sheria.  

Mheshimiwa Biteko aliwataka wananchi na viongozi wa mgodi huo kuheshimu sheria za nchi na kuzifuata na kupunguza migogoro isiyokuwa na tija baina ya wachimbaji na viongozi wa mgodi.

Aidha ameutaka mgodi huo kuchangia katika miradi ya maendeleo katika vijiji vinavyowazunguka kwa mujibu wa sheria. “Kuanzia kesho mgodi huu uanze kulipa mrahaba kwa mujibu wa sheria ili vijiji navyo viweze kupata chochote kutokana na uwepo wa mgodi hapa”. Alisema Biteko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa serikali ya Mkoa wa Mara imejipanga vizuri katika kushughulikia watu wote wanaofanya ubabe katika mgodi huo.

“Nimeambiwa katika mgodi huu kuna wababe hapa ambao wanajifanya kuwa wao ndio serikali sasa sisi katika Mkoa wa Mara tumejipanga vizuri, tutawanyoosha” alisema Malima.

Mheshimiwa amewataka wachimbaji hao kuchimba madini na kutafuta riziki yao vizuri kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.  

“Mimi ninatamani pawepo na uongozi unaoeleweka na kuheshimiwa na wote ili hata sisi wengine tuusikilize huo na sio kila mtu anakuwa kiongozi katika eneo hili” alisema Malima.

Mgodi wa Isaranilo unamilikiwa na wachimbaji wadogo wadogo na tayari una lesseni 15 ambazo zinatambulika kisheria lakini kwa siku za hivi karibuni umekumbwa na migogoro baina ya wachimbaji na wasimamizi wa mgodi huo.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.