• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Watumishi watakiwa kuzingatia maadili na taratibu za kazi

Posted on: July 30th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewataka watumishi wa Ofisi ya Mkoa wa Mara kuzingatia maadili na taratibu za kiutumishi katika utendajikazi wa kila siku.

Bwana Msovela ametoa kauli hiyo leo tarehe 29 Julai 2021 wakati alipokutana na wafanyakazi katika kikao cha kawaida cha wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji.

“Kila mtu atimize majukumu yake katika nafasi yake kulingana na sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma” alisema Bwana Msovela.

Amewataka watumishi kuzingatia mazuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na nidhamu katika utumishi wa umma na utendaji kazi kiufanisi ili kuleta tija katika kazi zao.

Aidha amewataka kuimarisha ushirikiano na mawasiliano kati ya viongozi na  watumishi wa ofisi hiyo katika kutekeleza majukumu yao.

Bwana Msovela amewataka watumishi kulipa umuhimu suala la kujikinga na maambukizi ya UVIKO 19 katika sehemu za kazi kwa kuvaa barakoa na kunawa maji au kutumia vitakasa mikono muda wote na kuzingatia maelekezo mengine ya wataalamu wa afya.

“Niwaombe tu mjiepushe na misongamano isiyo ya lazima kwa wakati huu na kuchukua tahadhari za mara kwa mara kuhusu UVIKO 19 ili tuendelee kubakia salama” alisema Bwana Msovela.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Mara unapakana na nchi jirani ya Kenya na Uganda na mikoa ambayo mingine inapakana pia na nchi nyingine na mwingiliano wa watu ni mkubwa sana kwa hiyo tahadhari ni muhimu kwa wakati huu.

Kikao cha Watumishi wa Mkoa wa Mara kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, Wakuu wa Idara na Vitengo na watumishi wote wa  Sekretarieti ya Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.