• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Watumishi wakumbushwa kutimiza wajibu wao

Posted on: April 8th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bwana Msalika Robert Makungu leo amekabidhi Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kwa Bwana Bwana Gerald Musabila Kusaya katika ukumbi wa uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo, Bwana Kusaya amewataka watendaji wa Serikali Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wananchi na kutoa ushirikiano baina yao na kwa viongozi katika utendaji kazi.

“Kila mtu kwenye nafasi yake akitimiza wajibu wake, kazi yangu itakuwa rahisi sana na kama kuna jambo limeshindikana, mimi nipo na kwa pamoja tunaweza kulitatua au kutafuta suluhisho kwa viongozi wengine wa Serikali” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amesema heshima ambayo watendaji wa umma wanaipata inatokana na nafasi waliyoipata na kuongeza kuwa vyeo ni dhamana na inahitaji kutimiza majukumu ili kuendelea kukitendea haki na kukiheshimisha cheo kilichopo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara pia amewataka wasimamizi wa kazi kwa nafasi mbalimbali za utumishi wa umma kuwasimamia watumishi waliochini yao na kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha, Bwana Kusaya amemshukuru Rais kwa kuendelea kumuamini na kuwashukuru viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Mara kwa mapokezi mazuri aliyoyapata tangu alipowasili kwa ajili ya kuanza kazi katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bwana Msalika Robert Makungu amewashukuru watumishi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano waliompa tangu alipoanza kutekeleza majukumu yake mwezi Agosti, 2022 hadi allipohamaishwa.

Bwana Makungu amewataka watumishi kumpa ushirikiano Katibu Tawala mpya ili umsaidie kuwahudumia vizuri wananchi wa Mkoa wa Mara.

Bwana Makungu ameongelea umuhimu wa kuimarisha menejimenti za Halmashauri (CMT) ili ziweze kushauri Mabaraza ya Madiwani kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi katika masuala mbalimbali.

Bwana Makungu ametumia fursa hiyo kuwakaribisha watumishi kuwekeza katika kilimo na ufugaji katika  Mkoa wa Rukwa.

 Hafla ya makabidhiano imehudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala Wasaidizi na Wakuu wa Vitengo, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na  watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.