• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Wasimamizi wa Elimu wahimizwa kutimiza wajibu

Posted on: December 19th, 2023

Mradi wa Shule Bora kwa kushirikiana na Wakala wa Mandeleo ya Elimu Tanzania (ADEM) wameendesha mafunzo ya siku moja ya wasimamizi wa Elimu katika ngazi mbalimbaliza Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ikiwa ni kuwajengea uwezo wasimamizi wa elimu kutekeleza majukumu yao.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi na wasimamizi wa shule kwa viongozi wa ngazi za Mkoa na Wilaya ya Serengeti yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Mapinduzi A, katika mji wa mugumu, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo Bwana Ayoub Mbilinyi amewataka wasimamizi hao kutimiza wajibu wao.

Bwana  Mbilinyi amewapongeza mwezeshaji wa mafunzo haya kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuwataka washiriki kuzingatia mafunzo hayo katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku.

Aidha, amewasistiza wasimamizi wa ngazi zote kuwasikiliza walimu na kutatua baadhi ya changamoto zao ili walimu wafundishe wakiwa na amani, na kufanya hivyo hakuhitaji fedha wala rasilimali nyingine ni kuwasikiliza tu. 

 Bwana Mbilinyi ametoa mfano kuwa kuna wakati Mkoa ulikuwa na makambi ya wanafunzi katika masomo mbalimbali na walimu waliokuwa wanafundisha wanafunzi walipewa chakula tu bila posho yoyote na kazi ilifanyika vizuri.

Bwana Mbilinyi amewataka wasimamizi wa elimu walioshiriki mafunzo hayo kuyasambaza kwa maafisa  wengine katika makundi tofauti tofauti ambao hawakubahatika kushiriki mafunzo hayo. 

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bwana James Johannes amewakaribisha washiriki na kuushukuru Mradi wa Shule Bora na wataalamu wa ADEM kuwapitisha wasimamizi wa elimu katika mafunzo ambayo walimu wakuu wa shule za msingi watafundishwa.

“Hii ni fursa kubwa kwetu kufundishwa angalau kwa juu juu kitu ambacho watu tunaowasimamia watafundishwa kwa muda wa siku tatu, haijawahi kutokea wasimamizi wafundishwe watakachoenda kufundishwa walimu wao, tunashukuru sana” amesema Mwal. Johannes.

 Aidha, Mwalimu Johannes amewataka washiriki kutumia fursa ya mafunzo haya kuongeza uelewa wao katika masuala muhimu ya kwenda kuyasimamia na kuwashukuru wakufunzi kwa kuwaelewesha kuhusu Jumuiya za kujifunza ambazo zitaundwa kwa ajili ya Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata. 

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.