• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Wananchi waaswa kuacha kulima kwenye vyanzo vya maji

Posted on: June 28th, 2022

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bwana Sahili Nyanzabara Geraruma amewataka wananchi wa Kata ya Itiriyo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuacha kulima katika chanzo cha maji ili mradi wa maji uliojengwa katika eneo hilo uweze kuleta matokeo yanayotarajiwa.

Bwana Geraruma ametoa agizo hilo leo akiwa katika eneo la Itiriyo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Itiriyo.

“Ninawaasa wananchi wanaolima karibu na chanzo cha maji cha mradi huu kuacha kabisa kulima eneo hilo kwa sababu chanzo kile kinatokana na chemichemi ambayo inaweza kukauka au kutoa maji kidogo kama chanzo hicho hakitatunzwa vizuri” alisema Bwana Geraruma.

Aidha Bwana Geraruma katika maeneo mbalimbali amewakumbusha wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi na kuachana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.  

Bwana Geraruma amewataka viongozi wa Wilaya ya Tarime kuhakikisha wananchi wanaacha kulima mara moja katika eneo hilo ili kulinda chanzo cha maji cha mradi wa maji wa Itiriyo.

Aidha Bwana Geraruma ameitaka Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) kuweka uzio katika eneo la chanzo na eneo lilipo tenki la maji na pampu yam aji ili kulinda miundombinu na vifaa vilivyopo katika maeneo hayo.

Wakati huo huo, mbio za Mwenge wa Uhuru zimeendelea leo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambapo ukiwa katika Halmashauri hiyo umeweka mawe ya msingi, kuzindua na kukagua miradi yote iliyokuwa imepangwa.

Miradi iliyowekewa mawe ya msingi ni pamoja na mradi wa maji Itiriyo, daraja la kebweye, Kituo cha Afya cha Bumera, na Shule mpya ya Sekondari Kata ya Sirari na umezindua Klabu ya Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari ya Nyamwigura.  

Aidha Mwenge wa Uhuru pia ukiwa katika Halmashauri hiyo umeteketeza madawa ya kulevya katika eneo la Turugeti-Runyerere na katika eneo la mkesha, Mwenge umekagua vikundi vya wanawake, vijana, walemavu, banda la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na shughuli za uhamasishaji wa wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Katika kuupokea Mwenge wa Uhuru, wananchi wengi sana walijitokeza na kubeba matawi ya miti kushangilia Mwenge wa Uhuru kuanzia eneo la makabidhiano hadi eneo la mkesha.

Mwenge wa Uhuru kesho tarehe 29 Juni, 2022 utaendelea na mbio zake katika Halmashauri ya Mji wa Tarime.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.