• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Wananchi wa Nyatwali waanza kupokea fidia

Posted on: September 10th, 2024

Zaidi ya wananchi 3,500 wa Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda wanaohama kupisha eneo la ushoroba wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) leo tarehe 9 Septemba, 2024 wameanza kulipwa fidia zao zoezi lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Dkt. Vincent Naano Anney.

Akizungumza wakati wa kuanza kwa utoaji wa malipo ya fidia Dkt. Anney amemshukuru Rais kwa kuamua kulipa fidia za wananchi mapema ili waweze kuendelea na shughuli zao za maendeleo katika sehemu nyingine.

“Jambo hili lilichukua muda mrefu lakini sasa limefikia mwisho wake, niwaombe wananchi mkishachukua fidia muanze kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo mapya ili kuzitumia fedha hizi kabla ya kuzitumia katika mambo yasiyo na msingi” amesema Mhe. Anney.

Aidha, amezitaka familia zenye migogoro kuhusu umiliki wa ardhi katika eneo hilo kumaliza migogoro hiyo haraka ili waweze kulipwa fidia zao na kuendelea na maisha mengine.

Kwa upande wake, Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Bwana Mussa Kuji ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kuwafidia wananchi wa Kata ya Nyatwali na kuwapongeza wananchi kwa kukubali kufidiwa ili kupisha shughuli za uhifadhi katika eneo hilo.

“Tuko kwenye zoezi muhimu sana, nimefurahi kuona wananchi wako tayari kufidiwa na kuruhusu kuachia eneo hili ili kutumika katika shughuli za uhifadhi” amesema Bwana Kuji.

Bwana kuji amewapongeza wananchi kwa kuonyesha umoja na mshikamano na kuongeza kuwa wananchi wengi alioongea nao wamefurahia kulipwa fidia na kwenda sehemu nyingine yenye amani na utulivu na kuondokana na usumbufu wa wanyama wakali katika makazi yao.   

Bwana Kuji amesema kwa sasa ikolojia ya Serengeti imerudi nah ii itaongeza utalii kw aupande wa magharibi na inategemea kuongeza watalii milioni 5 na kuleta mapato ya dola za kimarekani bilioni 6 ifikapo 2025.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa hundi ya malipo, Bi. Mgesi Kisuka Mchiro, Mkazi wa Mtaa wa Tamau ameishukuru Serikali kwa kutekeleza ahadi yake ya kutoa fidia na kwamba sasa familia yake itaondokana na adha ya wanyama wakali waliyokuwa wanaipata katika eneo hilo.

Kata ya Nyatwali ipo magharibi mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na wananchi wake wameanza kulipwa ili kupisha uhifadhi na uendelezaji wa eneo hilo ambalo ni mapito ya wanyama na hususan wakati wa kiangazi wanapoenda kunywa maji Ziwa Victoria pembezoni mwa Barabara ya Mwanza –Musoma.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.