• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Wadau toeni ushirikiano kwa TEMESA

Posted on: December 19th, 2023

Uongozi wa Mkoa wa Mara umeyataka taasisi na mashirika ya umma yaliyopo katika Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ili waweze kutoa huduma bora na endelevu.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa TEMESA katika Mkoa wa Mara uliofanyika leo katika ukumbi wa Mwembeni Complex kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalfan Haule amesema kuwa pamoja na Serikali kufanya maboresho makubwa katika utendaji wa TEMESA, wadau wasipotoa ushirikiano na huduma haziwezi kuimarika.

“Taasisi zote zikilipa madeni yake wanayodaiwa na TEMESA kwa wakati, TEMESA itaweza kuwalipa wazabuni wake na kuimarisha utendaji wake na hivyo taasisi nazo zitapata huduma bora zinazotegemewa” amesema Dkt. Haule.

Mhe. Haule ameipongeza TEMESA kwa  kuchukua hatua ya kujifanyia tathmini kwanza kabla ya kukutana na wadau ili kuwapa nafasi na wao kutoa maoni yao kuhusu shughuli zinazofaywa na wakala huyo katika maeneo yao ili waweze kuboresha.

Aidha, Mhe. Haule ameipongeza TEMESA kwa kuamua kufanya mabadiliko chanya katika utendaji wao na hususan kwa kuwekeza katika vifaa na rasilimali watu ili kuboresha huduma wanazozitoa kwa taasisi mbalimbali za Serikali hapa nchini.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TEMESA Bwana Lazaro Kilahala ameeleza kuwa TEMESA ilianza kufanyakazi mwaka 1925 kama Idara ndani ya Wizara inayohusika na Ujenzi na baadaye kuanzishwa Wakala unaojitegemea mwaka 2006.

“Kwa sasa tumeamua kama Wakala kubadilika, na kutokana na mabadiliko hayo tumeanza kuwekeana makubaliano ya kimkataba na taasisi mbalimbali za Serikali kutoa huduma za matengenezo ya magari ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na taasisi nyingine” amesema Bwana Kilahala.

Bwana Kilahala pia ameeleza kuwa kwa sasa Wakala inanunua vilainishi na vifaa vya umeme moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji ili kupunguza gharama na kudhibiti ubora wa vifaa wanavyotumia katika matengenezo.

Bwana Kilahala ameeleza kuwa kwa sasa Wakala hiyo inzo karakana 27 na vivuko na inafanya shughuli zake kwa kusaidiana na watoa huduma walioainishwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Ameyataja majukumu ya TEMESA kuwa ni kufanya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali; kufanya matengenezo na usimikaji wa mifumo ya umeme, mabarafu, viyoyozi, na Elekroniki inayomilikiwa na Serikali; na uendeshaji na usimamizi wa vivuko vya Serikali. 

 Ameyataja majukumu mengine kuwa ni kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Serikali na Umma kwa ujumla katika nyanja za uhandisi wa mitambo, umeme, na elekroniki; na kukodisha mitambo mbalimbali kama vile mitambo ya kuzalisha kokoto na mitambo ya kazi za barabara.

 Kikao hiki kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Wakuu wa Idara na Vitendo, Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa, taasisi na mashirika ya umma, wazabuni  na wadau wengine wa TEMESA, Menejimenti na watumishi wa TEMESA. 

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.