• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Viongozi na Watumishi Mara watoa zawadi kwa wahitaji

Posted on: December 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 24 Desemba, 2022 amekabidhi zawadi kwa wahitaji wanaoishi katika vituo vitatu vya kulelea watu wanaoishi katika mazingira magumu zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni tatu zilizotokana na michango ya viongozi na watumishi wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mheshimiwa Mzee ameeeleza wazo la kutoa zawadi hizo lilitokana na kitendo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa zawadi kwa ajili ya wahanga wa ukatili katika Kituo cha Masanga.

“Moyo wa Mheshimiwa Rais kutoa msaada kwa vituo mbalimbali wakati huu umetuhamasisha na sisi kutoa msaada kwa wenye uhitaji wanaoishi katika vituo vingine vilivyopo katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewashukuru sana viongozi na watumishi wote walioitikia wito wa kuchangia fedha za kununua zawadi hizo na kuahidi wakati mwingine michango itaanza mapema zaidi na kuwashirikisha watu wengi zaidi.

Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi kutoa msaada wa hali na mali kwa vituo vinavyohifadhi watu wanaoishi katika mazingira magumu ili viweze kuwahudumia wahitaji wengi zaidi.  

Vituo vilivyopewa zawadi ya sikukuu ni pamoja na Musoma Children Home kilichopo katika Wilaya ya Musoma, Kituo cha Kulelea Wazee cha Nyabange na Kituo cha Nyumba Salama cha Matumaini ambacho kinawahifadhi watoto ambao ni wahanga wa ukatili vilivyopo katika Wilaya ya Butiama.

Zawadi za sikukuu zilizotolewa katika vituo hivyo ni pamoja na mbuzi, mchele, maharage, mahindi, pampasi, viungo, taulo za kike na sabuni.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, Katibu Tawala wa Wilaya ya Butiama, Kaimu Mkurugezi wa Wilaya ya Butiama na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wilaya ya Musoma na Wilaya ya Butiama. 

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.