• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Vijana changamkieni fursa

Posted on: July 27th, 2024

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru godfrey eliakimu mzava amewataka vijana kuachana na mambo yasiyo na tija wajiunge kwenye vikundi vy uzalishaji mali na kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Ndugu Mzava ametoa rai hiyo wakati akizungumza na vijana baada ya kukagua mradi wa kikundi cha vijana cha Eden Group katika Kijiji cha Muriba, Kata ya Muriba Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati Mwenge wa Uhuru ukiendelea na mbio zake katika Wilaya ya Tarime.

“Kikundi hiki kinaundwa na viwanja watano wenye elimu ya Chuo Kikuu na mmoja chuo cha kati ambao walijiunga na kukopeshwa shilingi milioni sita na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mwaka 2023 ambao mpaka sasa wamesharejesha fedha zote za Halmashauri na biashara yao inaendelea vizuri” amesema Bwana Mzava.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amewapongeza vijana hao kwa kuungana pamoja katika mambo ya kujiletea maendeleo na kuanzisha biashara ambayo inaendelea vizuri na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mikopo itakapofunguliwa tena, kikundi hicho kipewe kipaumbele.

Bwana Mzava amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutoa kipaumbele cha mikopo kwa vikundi vinavyowahi kurejesha mikopo ya makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kuendelea kufanya shughuli za uzalishaji mali na kupunguza tatizo la ajira katika jamii.  

Kwa upande wake, Katibu wa Kikundi cha Eden Group Bwana Amos Lameck Gisiri amesema kikundi hicho kilianzishwa mwaka 2022 na kusajiliwa na Halmashauri hiyo kikiwa na wanachama watano na kati yao wanne wakiume na mmoja wakike.

Bwana Gisiri amesema kikundi chao kinajishughulisha na biashara ya vifaa vya umeme wa majumbani na viwandani na kiliwahi kukopeshwa na Halmashauri mwaka 2023 ambapo walirejesha mkopo na kwa sasa biashara yao ina mtaji wa shilingi 7,200,000.

“Lengo la kikundi ni kuwa na kampuni kubwa ya uuzaji na usambazaji wa vifaa vya umeme Wilayani Tarime” amesema Bwana Gisiri na kuongeza kuwa kwa sasa pamoja na duka hilo wameshafungua duka jingine katika kijiji cha Gibaso na kutoa ufadhili wa elimu kwa kijana mmoja kusomea Chuo cha Lubondo Biharamulo.

Mwenge wa Uhuru unaendelea na Mbio zake katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime baada ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime Bibi Angelina Lubella Marko kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime Bwana Saul Mwaisenye katika Kijiji cha Kerende, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Miradi mingine ambayo imetembelewa na kukaguliwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ni pamoja na jengo la biashara la Nyamongo Plaza ambao umezinduliwa, mradi wa maji Nyangoto ambao umetembelewa kuangaliwa uendelevu wake baada ya kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, mradi wa Bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Nyamwaga.

Miradi mingine itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru leo ni nyumba ya mtumishi ya 2 in one katika Kituo cha Afya Magoto, ujenzi wa daraja la Kebweye na mradi wa uhifadhi wa mazingira katika Shule ya Sekondari ya Nyasaricho.

 Mkesha wa Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuwa katika Uwanja wa Tarafa katika eneo la Sirari na kesho Mwenge unatarajiwa kukabidhiwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.