• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Vijana Badilisheni fikra kuhusu ajira

Posted on: March 11th, 2020

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu Mheshimiwa Anthony Mavunde amewataka vijana hapa nchini kubadili mtazamo wao kuhusu ajira ili kuweza kuzifanya shughuli zao zinazowaingizia fedha kwa bidii na maarifa.

Mheshimiwa Mavunde ameeleza hayo katika Kongamano la Vijana wa Mikoa ya Simiyu, Mwanza na Mara lililoandaliwa na wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na wadau wengine lililofanyika katika Wilaya ya Butiama tarehe 10 Machi 2020.

Ameeleza kuwa kwa mujibu wa sera ya ajira, “ajira ni shughuli yoyote halali inayomwingizia mtu kipato”. Hata hivyo vijana wengi wanadhani kuwa ajira ni lazima aajiriwe na akae ofisini ndio waiheshimu.

Mheshimiwa Mavunde amesema serikali inampango kwa kushirikiana na wadau katika kuziibua, kuzitangaza na kuzigawa fursa kwa vijana wengi hapa nchini ili waweze kujiajiri.

Mheshimiwa Mavunde amesema vijana wengi wanakata tamaa mapema, katika shughuli zao wakipata changamoto kidogo tu wanakata tamaa. Amewataka washiriki wa kongamano hilo kulitendea haki kwa kujifunza na mwisho kuyafanyia kazi yale yote waliyojifunza.

Amewataka vijana kuchangamkia fursa za kilimo cha matunda na mbogamboga ambazo zinaonekana kuwa na soko kubwa ndani nan je ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Malima akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kuzungumza katika kongamano hilo, amesema vijana wanayonafasi kubwa sana ya kuweza kujiajiri katika kilimo na biashara nyinginezo.

Aidha amewataka vijana kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali ambavyo vitawasaidia kupata mtaji, ujuzi na masoko ya bidhaa watakazozalisha.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Buatiama Mheshimiwa Anna Rose Nyamubi ameshukuru kwa waandaaji kuleta kongamano hilo katika Wilaya ya Butiama wilaya ambayo inahistoria kwa ya Taifa la Tanzania.

“Hii wilaya ndiyo wilaya ambayo Rais wa Kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Nyerere alizaliwa na kuzikwa hapa” alisema Mhehsimiwa Nyamubi.

“Tunaushukuru sana uongozi wa Mkoa kwa kuamua kuleta kiwanda kikubwa cha maziwa na uwanja wa kudumu wa maonyesho ya Kilimo katika Wilaya ya Buatiama. Alisema maamuzi hayo yatatoa fursa kwa vijana wengi kupata ajira na kujifunza mambo mbalimbali kupitia fursa hizo.

Aliwataka vijana kuchangamkia fursa za kilimo, uvuvi na ufugaji ili kuweza kutengeneza kipato halali ambacho kitawawezesha kutimiza ndoto na malengo yao.  

 Kongamano hilo lilihudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Butiama na Chief Josephat Wanzagi, kiongozi wa Kabila la Wazanaki.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.