• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Uthamini wa eneo la Nyatwali umefikia zaidi ya asilimia 50

Posted on: January 26th, 2023

Zoezi la uthamini katika eneo la Ghuba ya Speke, katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi endelevu wa mfumo wa ikolojia wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na usalama wa wananchi linaendelea vizuri na kwa sasa limefikia asilimia 53.7 ya utekelezaji wake.

Akizungumza katika Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa zoezi la uthamini leo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu amewataka wataalamu wanaofanya uthamini huo kutoa taarifa za maendeleo ya kazi kila wiki kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kupata uelewa wa pamoja na kutoa mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa zoezi hilo Serikalini.    

“Ninataka kuanzia sasa, kila wiki Mkoa upate taarifa ya maendeleo ya zoezi la uthamini ili Mkoa uweze kupeleka taarifa za utekelezaji wa uthamini na maendeleo ya zoezi hili kila wiki” amesema Bwana Makungu.

Aidha Bwana Makungu amewataka wataalamu hao kuongeza kasi ya kufanya tathmini ili zoezi hilo liweze kukamilika kwa haraka na wananchi wa eneo la Nyatwali waweze kulipwa fidia zao na kuendelea na shughuli zao za kawaida.  

Taarifa ya wataalamu inaonyesha kuwa mpaka hadi kufikia tarehe 25 Januari, 2023 jumla ya wananchi 2,175 wametambuliwa na kufanyiwa uthamini kati ya watu 4,050 waliokadiriwa hapo awali ambayo ni sawa na asilimia 53.7 ya uthamini wote.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa zoezi la uthamini lilianza Novemba, 2022 na linatarajiwa kukamilika Machi, 2023 na mpaka sasa jumla ya fomu 2,822 kati ya 4,050 zilizokadiriwa zimechukuliwa na wananchi ambayo ni sawa na asilimia 69.68 ya makadirio ya awali.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi la uthamini katika eneo hilo ni la hiari na kabla ya kuanza lilitanguliwa na mikutano na vikao vya uhamasishaji kwa viongozi na wananchi wa Kata ya Nyatwali na Wilaya ya Bunda kwa ujumla.

Utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa kutwaa eneo la Ghuba ya Speke lenye ukubwa wa ekari 14,250 kwa manufaa ya umma unahusisha Mitaa ya Tamau, Nyatwali, Kariakoo na Serengeti iliyopo katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda katika Mkoa wa Mara.

Utwaaji wa eneo la Ghuba ya Speke, utaunganisha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Ziwa Victoria na kuongeza ukubwa, uzuri wa mandhari ya vivutio vya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.  

Kikao cha kupokea maendeleo ya uthamini kimehudhriwa pia na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Wakuu wa Idara na Vitengo vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na baadhi ya wataalamu wa wanaohusika na zoezi la uthamini katika Ghuba ya Speke.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.