• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

TANAPA kuboresha Shule ya Msingi ya Kenyamusabi

Posted on: March 5th, 2021

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) imeahidi kuiboresha Shule ya Msingi Kenyamusabi iliyopo katika Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara ikiwa ni sehemu ya maridhiano kati ya wananchi na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Kanda ya Magharibi wa TANAPA Bwana Martin Loibooki ameeleza kuwa kwa kuanzia TANAPA itatoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya kumalizia vyumba viwili vya madarasa vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi katika shule hiyo.

“Mpango wetu ni kutenga fedha zaidi kwa ajili ya kujenga vyumba zaidi vya madarasa na kuyakarabati majengo ya shule yaliyopo katika bajeti ya TANAPA ya mwaka 2021/2022 ambayo inaendelea kuandaliwa” alisema Bwana Loibooki.

Aidha ameeleza kuwa TANAPA inampango wa kuendelea kuimarisha mahusiano na wananchi wa eneo hilo ambalo limekuwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya wananchi na SENAPA kutokana na masuala ya kugombea mipaka, uwindaji haramu ndani ya hifadhi, wananchi kuharibu miradi iliyotengenezwa na SENAPA nakadhalika.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ambaye aliongoza kikao hicho cha maridhiano leo tarehe 3 Machi 2021 ameeleza kuwa wananchi wakishiriki ipasavyo kwenye ulinzi wa hifadhi ya Serengeti watafaidika na mambo mengi sana ikiwemo uboreshaji wa huduma za kijamii katika eneo hilo.

“Nimefurahishwa sana na TANAPA kukubali ombi la wananchi la kuiboresha shule hii ili wananchi na watoto wanaosoma hapa waone kuwa wanafaidika na kuwepo kwa hifadhi karibu na maeneo yao na sio hadithi tu”alisema Mheshimiwa Malima.   

Aidha Mheshimiwa Malima amewahakikishia wananchi kuwa uchunguzi wa tukio la kupotea kwa Bwana Manga Kahuru Manga unaendelea na timu ya wataalamu wanaendelea kuchunguza na matokeo ya uchunguzi yatawasilishwa kwao mara baada ya uchunguzi kukamilika.

“Ninawaomba muendelee kutoa ushirikiano kwa timu ya uchunguzi  wa tukio hilo ili tuweze kupata ufumbuzi wa tukio la kupotea kwa kijana huyu kwa haraka” alisema Mheshimiwa Malima.

Kijana Manga Kahuru Manga mwenye umri wa miaka 20 alipotea wakati akiwa anachunga ng’ombe na mwezie ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti tarehe 11 Desemba 2020 na mpaka sasa uchunguzi bado unaendelea.

Katika kikao hicho wananchi pamoja na diwani wa eneo hilo Mheshimiwa Ayoub Marwa walifurahishwa na ahadi hiyo ya TANAPA na kuahidi kutoa ushirikiano kwa TANAPA katika kuimarisha mahusiano yaliyopo kati ya hifadhi na wananchi wa eneo hilo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.