• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

TAMISEMI yaitaka Mara kuboresha ufaulu

Posted on: April 28th, 2020

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mara kuboresha kiwango cha ufaulu katika mitihani ya taifa kwa shule za msingi na sekondari. 

Eng. Nyamhanga ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti tofauti katika ziara yake ya siku tatu ya kutembelea Mkoa wa Mara na kukagua maendeleo katika sekta ya Elimu, Afya na utayari wa Mkoa katika kukabiliana na janga la homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

“Tumeiona mipango yenu na utekelezaji wake umeanza lakini tunahitaji ufaulu upande. Na sisi kwa upande wa wizara tumembadilisha Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara labda tutakuja kupata matokeo mazuri wakati huu” alisema Eng. Nyamhanga.

Katika kuunga mkono juhudi mbalimbali za wananchi na watendaji wa Mkoa wa Mara, Katibu Mkuu TAMISEMI aliahidi kutoa fedha za kusaidia ukamilishaji wa maboma ya madarasa, nyumba za walimu na maabara katika shule mbalimbali alizozitembelea katika ziara hiyo.

Katika ziara yake ya Mkoa wa Mara, Katibu Mkuu TAMISEMI alitembelea shule za sekondari za Kebogwe, Tarime na Nyamigwela na Shule ya Msingi ya Nyasaricho katika wilaya ya Tarime; Sekondari za Mapinduzi, Mugumu na Natta katika Wilaya ya Serengeti; na Sekondari ya Kabasa katika Wilaya ya Bunda.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula ameahidi Mkoa kufanya vizuri kutokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na serikali pamoja na wadau wa Elimu katika Mkoa wa Mara.

“Kwa niaba ya watendaji wote wa Mkoa huu, tunashukuru sana wadau wetu mbalimbali ambao wamekuwa wakiunga mkono uboreshaji wa elimu katika Mkoa wa Mara” alisema Bibi Mthapula.

 Katibu Mkuu TAMISEMI ametembelea wilaya za Tarime, Serengeti na Bunda katika Mkoa wa Mara kukagua shughuli za maendeleo katika sekta za Afya, Elimu na kuangalia utayari wa mkoa katika kukabiliana na janga la Korona.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.