• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

TAKUKURU yatoa taarifa ya utekelezaji

Posted on: July 29th, 2022

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara leo tarehe 28 Julai, 2022 imetoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yake katika robo ya Aprili hadi Juni, 2022 na kueleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU imefuatilia utekelezaji wa miradi 24 ya maendeleo.  

Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Antony Gang’olo, ameeleza kuwa miradi iliyofuatiliwa ilikuwa na thamani ya shilingi 18,578,309,485 katika sekta za afya, barabara, maji na elimu.

“Katika ukaguzi huo, miradi mitatu ilibainika kuwa na changamoto ambazo zinaendelea kurekebishwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa chumba cha wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime; mradi wa maji wa Kijiji cha Robanda na mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Sekondari ya Mapinduzi katika Wilaya ya Serengeti” alisema Gang’olo.

Aidha, Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU imetembelea klabu za wapinga rushwa 86 katika Wilaya zote sita na kufanya mikutano ya hadhara 30 katika vijiji, mitaa na vitongoji mbalimbali katika Mkoa wa Mara.  

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho pia TAKUKURU imeshiriki katika vikao 15 na kutoa mada za kuelimisha umma pamoja na kushiriki vipindi vitatu katika vituo vya redio za kijamii za Victoria FM, Mazingira FM na Bunda FM.

Wakati huo huo, Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho, jumla ya malalamiko 106 na kati ya malalamiko hayo 79 yalihusu vitendo vya rushwa yanaendelea kufanyiwa kazi wakati 27 hayakuhusu vitendo vya rushwa.

“Kati ya malalamiko hayo, malalamiko 26 yalihusu TAMISEMI, 11 Afya, 07 Jeshi la Polisi, 06 sekta ya vuvi, 06 sekta ya ardhi na sekta nyinginezo” alisema Bwana Gang’olo.  

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho, uchunguzi katika majalada 18 ulikamilika na kesi 18 zilifunguliwa mahakamani na kufanya kesi zinazoendelea mahakamani kuwa 36 huku kesi tatu zikiamriwa ambapo kesi 2 washtakiwa walipatikana na hatia na kesi moja mshtakiwa aliachiwa huru.  

Ameeleza kuwa katika kipindi cha Julai- Septemba 2022 TAKUKURU Mkoa wa Mara itaongeza nguvu zaidi katika kuzuia vitendo vya rushwa na itashirikiana na Chama cha Skauti Tanzania kutekeleza mpango wa TAKUSKA unaolenga kutoa elimu ya rushwa kwa vijana wengi zaidi.  

Taarifa hii ya TAKUKURU ni mwendelezo wa taarifa zinazotolewa na TAKUKURU Mkoa wa Mara kwa waandishi wa habari kila baada ya miezi mitatu.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.