• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

TAKUKURU yafuatilia miradi ya maendeleo 32 Mara

Posted on: April 25th, 2024

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara leo imetoa taarifa yake ya  utendaji kwa kipindi cha Januari, 2024 hadi Machi, 2024 ambapo imefuatilia miradi ya maendeleo 32 yenye thamani ya shilingi 11,372,416,636.5 inayotekelezwa na Serikali katika sekta za elimu, afya, barabara na maji.

Taarifa iliyotolewa leo na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Mohamed Shariff imeeleza kuwa uchunguzi wa awali ulibaini dosari katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Bunda yenye thamani ya shilingi bilioni nne.

“Tayari Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imerekebisha dosari zilizoonekana ikiwa ni pamoja na kuta zilizokuwa zimepinda kwenye vyumba vya madarasa, nyufa kwenye mabweni, fundi amekatwa shilingi 360,000 kufidia simenti iliyotumika kutengeneza ukuta mnene uliozidi katika ujenzi wa bweni na vitabu vya stoo vilivyokuwa havijazwi kwa sasa vinajazwa” amesema Bwana Shariff.

 TAKUKURU imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kuyafanyia kazi mapungufu yaliyoonekana kwa wakati hata hivyo uchunguzi wa kina kuhusiana na shule hiyo bado unaendelea.

Bwana Shariff ameeleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU ilipokea malalamiko 103, kati ya hayo malalamiko 57 yalihusu vitendo vya rushwa na 46 hayakuhusu vitendo vya rushwa na kesi moja ilifunguliwa mahakamani na kesi moja iliyokuwa mahakamani imeamriwa na Jamhuri kupata ushindi.

Aidha, TAKUKURU ilifanya uchambuzi wa mifumo ya utoaji na usimamizi ya adhabu katika Shule ya Sekondari ya Nyamunga katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya baada ya kupokea malalamiko ya kuwatoza wanafunzi wanaokamatwa na simu shilingi 200,000.

Bwana Shariff ameeleza kuwa katika kipindi hicho pia TAKUKURU imefanya uelimishaji umma kupitia klabu za wapinga rushwa 30 kutoka shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati, mikutano ya hadhara 31 na semina 20.  

 Kwa mujibu wa Bwana Shariff, mkazo uliwekwa katika uzuiaji wa vitendo vya rushwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, utoaji wa huduma na kuwashirikisha wadau katika mapambano dhidi ya rushwa na jumla ya wananchi waliopatiwa elimu kuhusu rushwa katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara ni 6,220.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.