• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Simbachawene kufanya ziara Mkoa wa Mara

Posted on: October 1st, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene leo anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku nne katika Mkoa wa Mara ambapo atakagua na kutembelea miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, baada ya kupokelewa Mhe. Simbachawene anategemewa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, kuzindua vyumba 13 vya madarasa, matundu 17 ya vyoo na mabweni matano katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songe, kuzindua daraja katika Mtaa wa Majengo Mapya kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Sekondari Mara, Manispaa ya Musoma.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa kesho Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, kuzindua Shule ya Sekondari ya Ingri na kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Utegi Wilaya ya Rorya.  

Msafara utaelekea Wilaya ya Tarime, ambapo Mhe. Simbachawene atazindua Shule ya Msingi Komote na mradi wa maji Kemakorere na baadaye kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Kemakorere.

Tarehe 3 Oktoba, 2024 Mhe. Simbachawene anategemea kuzindua Zahanati ya Getarungu na kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Getarungu, kuweka jiwe la msingi katika barabara ya Stendi Mpya katika mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti.

Baada ya hapo msafara unatarajiwa kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuzindua Shule ya Msingi ya chifu Manyori na kufanya mkutano wa hadhara katika stendi ya mabasi katika eneo la Nyamisisi.

Tarehe 4 Oktoba, 2024 Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Zahanati ya Nambaza, kutembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara na kuzindua Shule ya Sekondari ya Bunda Mjini kabla ya kuhitimisha ziara hiyo na mkutano wa hadhara katika eneo la Stendi ya Zamani iliyopo katika Mji wa Bunda.

Mhe. Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, lililopo katika Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma katika ziara hii anatarajiwa pia kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.