• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Shule bora yatoa mafunzo ufundishaji kiingereza

Posted on: December 19th, 2023

Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata ambao shule zao zilifanya vibaya kwenye Somo la Kiingereza katika mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba mwaka 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti leo tarehe 27 Novemba, 2023 wamepewa mafunzo ya namna ya kusimamia ufundishaji wa somo hilo yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Azimio A. 

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Mujibu Mustafa Babara ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu na kuwataka washiriki wa mafunzo kufuatilia mafunzo hayo ili kwenda kubadilisha hali ya ufundishaji wa somo hilo.

“Tunataka mkimaliza mafunzo hayo, mabadiliko ya wazi yaonekani kwa namna walimu wenu watakavyokuwa wanafundisha na namna wanafunzi watakavyoongeza ufaulu wa asomo la kiingereza katika shule zenu” amesema Bwana Babara.

Bwana Babara ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara wataalamu hao watakuwa wakwanza kupewa mafunzo ya kusimamia na kutekeleza muhutasari wa somo la Kiingereza kwa shule za Msingi kulingana na Mtaala wa Elimu ya Msingi, 2023.

“Ninyi mnapewa mafunzo kwenye mada mpya kabisa ambayo nina uhakika sio walimu wote hapa nchini watapata fursa mliyoipata leo, tuyatendee haki haya mafunzo na tukawajibike katika kuwasimamia walimu wanaofundisha” amesema Bwana Babara.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Bwana Sam Mwita ameeleza kuwa ufaulu wa somo la Kiingereza kitaifa ni asilimia 34 na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ilikuwa ni ya mwisho katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba, 2023.

“Ni mategemeo yetu kuwa mafunzo haya, na mafunzo yatakayotolewa kwa waliu kesho yataboresha ufundishaji wa wanafunzi na hivyo kuja kuboresha matokeo ya somo la kiingereza katika mitihani ya ndani na mitihani ya Taifa” amesema Bwana Mwita.

Bwana Mwita ameelezea imani yake kuwa walimu hao wanaouwezo wa kufanya mabadiliko na wanasifa za kufanya mabadiliko na kuwataka kutekeleza kwa ufanisi mpangokazi watakaotoka nao katika mafunzo hayo.

Kwa upande wake, Mdhibiti Ubora wa Kanda ya Ziwa Bibi Lucy Nyanda ameeleza kuwa kuna mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu na hivyo walimu hawana budi kujifunza kuhusu mtaala na sera mpya za elimu zilizoanza kutumika hivi karibuni.

Bibi Nyanda amewataka washiriki hao kuchukulia mafunzo hayo kama chachu ya kujifunza mambo yote yanayohusiana na elimu na mabadiliko ya mitaala na sera ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mafunzo ya Wakuu wa Shule na Maafisa Elimu Kata yanatarajiwa kufuatiwa na mafunzo kwa walimu wanaofundisha somo la Kiingereza katika shule hizo yanayotarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Novemba, 2023.

 Mafunzo haya yanatolewa na Wakala wa Maendeleo ya Elimu (ADEM) na kufadhiliwa na Mradi wa Shule Bora.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.