• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikari inathamini mchango wa wafanyabiashara wadogo

Posted on: February 18th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo (16 Februari, 2024 amefungua mafunzo ya siku moja ya Maafisa biashara, Tehama na Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Mara kuhusu mfumo wa kuwatambua na kuwasajiri wafanyabiashara wadogo yaliyofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Musoma.

Akizungumza katika halfa ya ufunguzi wa mafunzo hayo, Bwana Makungu amesema dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kujenga mazingira wenzeshi ya wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) kufanya biashara zao ili kujipatia kipato kwa maendeleo yao na jamii kwa ujumla.

“Tangu nchi yetu ipate uhuru, kwa mara ya kwanza Serikali ya awamu ya sita inajenga ofisi kila Mkoa kwa ajili ya viongozi wa chama cha wafanyabiashara wadogo hapa nchini na inaanzisha mfumo rasmi wa kuwatambua na kuwasajiri kama kundi muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amewataka wataalamu watakaohusika kuwatambua na kuwasajiri wafanyabiashara wadogo kufanyakazi hiyo kwa umakini na kwa uzalendo ili kutoa nafasi kwa walengwa wa kundi hili kutambuliwa kiurahisi.

Bwana Makungu ameeleza kuwa mfumo huu umekuja ili kuboresha mfumo wa awali wa utoaji wa kuwatambua na kuwahudumia wafanyabiashara wadogo hapa nchini kutokana na umuhimu wa kundi hilo kwa maendeleo ya nchi yetu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Viwanda Bwana Timotheo Gambaless ameeleza kuwa mfumo huo wa kielekroniki utawezesha kupata taarifa za utambulisho wa uraia, taarifa za watu wa karibu na mfanyabiashara huyi na aina ya biashara na sehemu biashara inapofanyika.

Bwana Gambaless ameeleza kuwa katika mfumo huu mpya wafanyabiashara watalipia shilingi 20,000/= kama awali lakini kitambulisho atakachopatiwa kitatumika eneo lolote hapa nchini bila kuhitaji kujisajiri tena.

Aidha, Mfumo huu utakapokamilika utaiwezesha Serikali kuwatambua na kufuatilia taarifa mbalimbali za wafanyabiashara wadogo hapa nchini na kufuatilia maendeleo yao na namna wanavyokua kibiashara hadi kuwa wafanyabiashara wakubwa.  

 Mafunzo haya ya siku moja yameendeshwa na Wizara ya Viwanda na Biashara na kuhudhuliwa na maafisa Tehama, Biashara na Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.