• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikali yawataka wafugaji kuboresha mifugo kukuza uchumi

Posted on: June 6th, 2024

Serikali ya Mkoa wa Mara imewataka wafugaji kufuga kisasa na kuboresha mifugo yao ili kuwawezesha kupata soko la uhakika la mifugo na mazao ya mifugo yao ili kuboresha uchumi wa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa leo katika hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi iliyosomwa kwa niaba yake na Mhe. Moses Kaegele, Mkuu wa Wilaya ya Butiama katika uzinduzi wa Nyama Choma Festival iliyofanyika katika mnada wa Kiabakari Wilaya ya Butiama.

“Wafugaji wakifuga kisasa watasaidia kupata mifugo iliyo bora na nyama bora ambayo itawawezesha kupata soko la uhakikika kwa ndani na nje ya nchi” amesema Mwalimu Kaegele.

Mhe. Kaegele amesema Mkoa wa Mara unayo mifugo mingi ambayo ikitumika vuzuri itakuza uchumi wa wananchi na Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla na kuwataka wananchi kuchangamkia ufugaji wa kisasa wa mifugo.

Mwalimu Kaegele ameeleza kuwa mashindano hayo ni endelevu na yameanza katika Wilaya ya Butiama na yatafanyika katika Wilaya nyingine za Mkoa wa Mara lengo likiwa kuwapata wachoma nyama mahiri ambao watatumika katika kuchoma nyama katika matukio mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Mara.

“Mkoa utayatumia mashindano haya kuwatangaza wachoma nyama mahiri waliopo katika Mkoa wa Mara ili waweze kutumika katika matukio mbalimbali ya ndani na nje ya Mkoa katika matukio mbalimbali” amesema Mhe. Kaegele.

Mhe. Kaegele amewataka wananchi kudumisha amani, utulivu na usalama ili kuweza kuwavutia watu zaidi wengi zaidi kushiriki katika mashindano hayo na kuwekeza katika Wilaya ya Butiama kufuatia Serikali kuanzisha Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Technolojia (MJNUAT) Butiama ambacho kinategemewa kuanza kudahili wanafunzi 4,000 kwa mwaka hivi karibuni.

Bwana Kaegele ameeleza kuwa uwekezaji unaohitajika zaidi ni mahoteli, mabweni ya wanafunzi, nyumba na usafiri kwa ajili ya ongezeko kubwa la idadi ya watu linalotegemewa baada ya ujenzi wa Chuo hicho kukamilika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama  Mhe. Christopher  Marwa Siagi amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kwa kuanzisha mashindano hayo ambayo yakifanyika vizuri yanaweza kuutangaza Mkoa wa Mara kwa namna ya kipekee.

Mhe. Siagi ameeleza kuwa tukio hilo limepata mwitikio mkubwa japokuwa linafanyika kwa mara ya kwanza na kutangazwa ndani ya muda mfupi ni kutokana na umuhimu wake kwa wajasiriamali na mahitaji halisi ya wananchi wa Mkoa wa Mara.

 Mashindano hayo yamehudhuriwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama Wilaya ya Butiama, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Butiama, baadhi ya maafisa kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, taasisi za umma zilizopo Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.