• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikali yatoa maamuzi matumizi ya CSR Tarime

Posted on: July 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 13 Julai, 2022 ametoa mrejesho wa maamuzi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) kuhusu fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara.

Akizungumza katika kikao cha Baraza Maalum la Madiwani la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa maamuzi ya Waziri Mkuu yalitolewa katika kikao cha pamoja kilichowahusisha viongozi wa serikali wa ngazi mbalimbali, Mbunge wa Tarime Vijijini na viongozi wa Mgodi wa Barrick North Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa maamuzi ya kikao hicho yalikuwa fedha zote za CSR zinazotolewa na mgodi huo ni mali ya umma na matumizi ya fedha hizo lazima yafuate taratibu zote za fedha za Serikali za mitaa. 

“Serikali imeamua kuwa hakutakuwa tena na Kamati ya Maendeleo ya Jamii (CDC) iliyokuwa ikitumika  kupanga na kutekeleza miradi ya CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na badala yake miradi yote itatekelezwa kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya kawaida ya serikali” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Wataalamu watapata fursa ya kuchambua miradi iliyoibuliwa na kufanya michakato ya kitaalamu kuhusiana na miradi hiyo kabla ya kuiwasilisha kwenye mamlaka za maamuzi kwa ajili ya kuidhinisha utekelezaji wa miradi hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mfumo wa malipo ya fedha hizo itakuwa sawa na fedha zote za Serikali na zitapelekwa kwenye Kata ambapo mradi unatekelezwa na taratibu zote za fedha na manunuzi ya umma zitafuatwa katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa kuanzia sasa Serikali kwa maana ya Mkoa na Halmashauri utashiriki kwenye kukokotoa kiwango cha CSR kitakacholipwa na mgodi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tarime sio kama ilivyokuwa awali halmashauri ilikuwa ikipatiwa taarifa tu na mgodi kuhusu kiasi cha CSR.  

Aidha, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa fedha ya CSR itatolewa kwa Dola za Kimarekani na Halmashauri ndio itakayehusika katika kubadilisha dola hizo kuwa fedha za kitanzania kwa ajili ya matumizi ya Halmashauri.

“Huu utaratibu wa matumizi ya CSR umekubalika kuwa ni utaratibu wa nchi nzima baada ya kikao kilichofanyika chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Maamuzi haya ya Serikali yanahitimisha malumbano ya matumizi ya fedha CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime yaliyodumu kwa muda mrefu kufuatia uongozi wa Mkoa wa Mara kuingilia kati matumizi ya fedha hizo na kuunda kamati maalum ambayo iliwasilisha taarifa yake tarehe 20 Aprili, 2022.

Hata hivyo kulikuwepo na malalamiko ya wananchi na wanasiasa hususan baada ya kuvunjwa kwa CDC tarehe 20 Aprili, 2022 na vyombo vya dola kuanza uchunguzi kutokana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za CSR za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.