• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikali kuubadilisha Musoma kuwa Mji wa Utalii

Posted on: September 11th, 2020

Uwekezaji katika upanuzi na uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Musoma unaofanywa na serikali ya unalenga kuubadilisha mji wa Musoma kuwa mji wa Utalii na Mkoa wa Mara kuwa ndio lango kuu la kuingilia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 11 Septemba 2020.

“Uwanja wa ndege wa Musoma utakapokamilika utaleta ndege za Shirika la Ndege la Tanzania na ndege nyingine ambazo zitaleta watalii kwa wingi hususan katika msimu wa watalii” alisema Mheshimiwa Malima.

Amewahamasisha wafanyabiashara kuwekeza zaidi katika huduma za kuwahudumia watalii ili uwanja utakapokamilika kuwe na huduma za kuwapa watalii.

Amezitaja huduma hizo kuwa ni pamoja na chakula, mahoteli, mabenki, hospitali, usafiri, na kadhalika ambazo zitawafanya watalii kufurahia kuwepo Tanzania na hivyo kutamani kurudi tena.

Aidha amewataka wakazi wa Mkoa wa Mara kubadilisha mtazamo wao na kuanzisha ukarimu kwa wageni ili waweze kufaidika na fursa za utalii zilizomo katika Mkoa wa Mara.

“Mara ndio sehemu pekee ambapo Serengeti inakutana na Ziwa Victoria, wanyama wanapovukia kwenda Masai Mara, Kenya, Nyumbu wanapozaliana na kadhalika, tukiendelea na tabia zetu mbaya zitawatisha watalii na tutabakia kuwa nyuma kimaendeleo” alisema Malima.

Aidha amehimiza uwekezaji katika miji mingine ya Mugumu, Bunda na Natta ili kuweza kuwapokea na kuwahudumia watalii wanaotegemewa kuja baada ya uwanja wa ndege kukamilika Musoma.

Mheshimiwa Malima alisema Rais ametoa ahadi ya kukamilisha uwanja huo kutokana na umuhimu wake kwa Mkoa wa Mara lakini pia kwa ukuaji wa sekta ya utalii hapa nchini.

Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alitoa ahadi ya kukamilisha uwanja wa ndege wa Musoma tarehe 5 Septemba 2020 katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mukendo katika Manispaa ya Musoma.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.