• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikali kuendelea kuunga mkono shughuli za wanawake hapa nchini

Posted on: February 14th, 2025

Mkuu wa mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefungua Mkutano wa Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Mkoa wa Mara na kuwahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuunga mkono shughuli za wanawake hapa nchini.

Mhe. Mtambi ameeleza hayo leo Februari 14, 2025 katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati akizungumza na wanawake takriban 200 wanachama wa Chemba ya Wanawake Tanzania.

“Serikali inazo fursa nyingi kwa ajili ya wanawake ikiwemo mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa hapa nchini kwa ajili ya makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu” amesema Mhe Mtambi.

Mhe. Mtambi pia amesema Serikali imeweka mazingira mazuri ikiwemo sera, sheria, kanuni na taratibu zinazowawezesha wanawake kufanya shughuli zao na hususan shughuli za uzalishaji mali bila kubaguliwa.  

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo pia kuwakumbusha wanawake wa Mkoa wa Mara kuhusu fursa mbalimbali zilizopo katika Mkoa wa Mara ikiwa ni pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii na uchimbaji wa madini.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kuhakikisha kuwa katika maonesho ya Kitaifa na Kimataifa wanawake wa Mkoa wa Mara wanapata nafasi na wanashiriki.  

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka wanawake wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja na kuwania nafasi mbalimbali zinazogombaniwa na kupiga kura ili kumchagua Rais, wabunge na madiwani.  

Awali, akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Katibu wa Chemba ya wanawake Mkoa wa Mara Bi Anastazia Kirati amesema wanawake wajasiriamali wanapata changamoto katika kupata mikopo kutoka Serikalini na taasisi za kifedha.

“Wanawake wanapata changamoto ya kupata mikopo ambapo wapo wanaopata lakini hawana fursa ya elimu ya kutosha na hivyo kuwafanya kushindwa kuitumia vizuri mikopo hiyo.” Amesema Bi. Anastazia.

Bi. Anastazia ameiomba Serikali na taasisi za kifedha kutoa elimu ya biashara kwa wajasiriamali wanaopewa mikopo ili waweze kufaidika zaidi na mikopo hiyo kwa kuendeleza biashara zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kanda wa TWCC Bi Happines Mabula amesema kuwa chemba yao ilianzishwa mwaka 2005 sasa inakaribia kuwa na miaka 20 ikitoa huduma zake kwa wananwake wafanyabiashara na wajasiriamali hapa nchini.

Ufunguzi wa mkutano huo umehudhuriwa pia na baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.