• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Serikali inampango wa kuibadilisha Musoma

Posted on: October 2nd, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene leo amefanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Mara na kuzungumzia mpango wa Serikali kufanya uwekezaji mkubwa wa miundombinu ili kuibadilisha Manispaa ya Musoma.

Akiwahutubia wananchi wa Musoma, Mhe Simbachawene amesema katika mipango yake Serikali inampango wa kupanua treni ya kisasa ya SGR ifike Musoma, kujenga bandari kubwa na uwanja wa ndege wa kimataifa na miradi hii ikikamilika itaibadilisha kabisa Manispaa ya Musoma.

“Miradi hii haitafanywa kwa pamoja itafanywa kwa awamu ya miaka mitano mitano ili kuvutia watalii zaidi kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuimarisha uchumi wa Mkoa wa Mara kwa kuufugua mkoa huu katika sekta ya usafirishaji” amesema Mhe. Simbachawene.

Akizungumzia kuhusu treni ya SGR, Mhe. Simbachawene amesema mpango wa Serikali baada ya treni hiyo kufika Mwanza, kutakuwa na mradi mwingine wa kujenga treni hiyo kuja Musoma na  itaunganishwa kuelekea Kenya, lengo likiwa ni kurahisisha usafirishaji wa  mizigo ambayo itapunguza bei za bidhaa baada ya kufika Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema Serikali pia inampango wa kupanua na kuimarisha Bandari ya Musoma ili kuvutia meli kubwa kuweza kuta nanga katika bandari hiyo na kuimarisha usafirishaji wa mizigo na abiria na uchumi wa Manispaa ya Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema Serikali inampango wa kujenga uwanja wa ndege wa Kimataifa baada ya kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa uwanja uliopo ili kuwavutia watalii wengi zaidi kuingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kupitia uwanja huo wa Musoma.

Mhe. Simbachawene amesema kwa sasa Mkoa wa Mara umekuwa ukipokea watalii wengi wanaoingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kutambua kuwa ni rahisi kuingia ukitokea Wilaya za Bunda na Serengeti.

Mhe. Simbachawene amesema ndani ya miaka mitatu Mkoa umepata fedha nyingi kutokana na ongezeko la watalii kuliko wakati mwingine wowote.

Wakati huo huo, Mhe. Simbachawene amewataka vijana kutokuyumbishwa na watu wasiopenda maendeleo na badala yake kuchukua fursa hiyo kufuatilia mambo yanayofanywa na Serikali na taasisi zake katika kuwaletea wananchi huduma mbalimbali za maendeleo.

Mhe. Simbachawene amesema kwa kasi ya maendeleo inayofanyika hapa nchini, amani na utulivu ukiendelea kwa miaka mingine 25, Tanzania itakuwa imepiga hatua kubwa sana katika maendeleo ya kiuchumi, hivyo amewataka vijana kuilinda amani kwa nguvu zao zote.

Aidha, amewataka vijana kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na Serikali Kuu wa mwaka 2025 ili kuwachagua viongozi bora wanaopenda maendeleo kuanzia kwenye mitaa, vijiji na vitongoji vyao hadi Taifa.

 Ziara ya Mhe. Simbachawene inatarajiwa kuendelea kesho katika Wilaya za Rorya na Tarime na tarehe 3 Oktoba, 2024 katika Wilaya ya Serengeti na Butiama na kuhitimishwa tarehe 4 Oktoba, 2024 katika Wilaya ya Bunda.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.