• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Sekondari ya Kibumaye ikamilike Mei, 2025- Mtambi

Posted on: April 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 11 Aprili, 2025 ametembelea ujenzi wa Shule ya Sekondari Kibumaye inayojengwa katika eneo la Mogabiri, Halmashauri ya Mji wa Tarime na kuagiza ujenzi wa shule hiyo ukamilike katikati ya mwezi Mei, 2025.

Akizungumza katika mradi huo, Mhe. Mtambi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime kuhakikisha kazi ya ujenzi inafanyika usiku na mchana na inakamilika ili kuiwezesha shule hiyo kuanza kuchukua wanafunzi.

“Mimi nitapita kukagua utekelezaji wa mradi huu katikati ya Mei, 2025 nikute umekamilika la sivyo nikute hatua zimechukuliwa kwa yoyote aliyehusika katika kuukwamisha mradi huu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhe. Meja Edward Gowele kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa mradi huo na kumpa taarifa za maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo mara kwa mara.

Akiwa katika eneo hilo Mhe. Mtambi ametembelea Shule ya Msingi Mogabiri na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime kukarabati ofisi ya walimu wa shule hiyo na kutoa muda wa kuanzia leo hadi katikati ya Mei, 2025 ukarabati uwe umekamilika.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kufuatilia na kutoa taarifa ndani ya siku 14 kuhusu zabuni zote alizopewa Mzabuni aliyefahamika kwa jina la Mama Leah katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa mzabuni huyo amepewa zabuni nyingi za kusambaza vifaa kwenye miradi inayotekelezwa katika Halmashauri nyingi za Mkoa wa Mara lakini hamna sehemu amefanya vizuri baada ya kushinda zabuni hizo kupitia kwenye mfumo wa NEST.

Akiwa katika Sekondari ya Julius Kambarage Nyerere, Mhe. Mtambi ameagiza mzabuni huyo asipewe zabuni nyingine mpya katika Mkoa wa Mara mpaka hapo atakapokamilisha utekelezaji wa zabuni alizonazo kwa sasa.

Mhe. Mtambi ametoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa kuwa mzabuni huyo amechelewesha pia utekelezaji wa mradi katika shule hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele amesema Mama Leah ameshinda zabuni katika miradi mingi inayotekelezwa katika Halmashauri za Wilaya ya Tarime na Mkoa wa Mara kwa ujumla na hana uwezo wa kusambaza vifaa hivyo kwa wakati.

“Kila alipopewa zabuni analalamikiwa kuwa hatekelezi kwa wakati na ameshinda zabuni nyingi katika miradi ya Serikali inayotekelezwa na Halmashauri za Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Gowele.

Kwa upande wake, Diwani wa eneo hilo Mhe. Daudi Mrimi Wangwe amesema mradi huo unachelewa kutokana na mzabuni wa vifaa kuwakwamisha mafundi ambapo mara kwa mara vifaa kama vile matofali, mawe, mchanga, nondo na kadhalika anachelewa kuleta na hivyo kukwamisha kazi.

“Haya majengo yapo tayari muda mrefu lakini yeye pia anachelewesha kuleta mbao za kupaulia na kila wakati anatoa ahadi ambazo hazitekelezi kama anavyoahidi” amesema Mhe. Wangwe.

Mhe. Wangwe amesema Kamati ya Ujenzi wa mradi huo inapomfuatilia mzabuni huyo anatoa majibu ya kejeli kwa kamati hiyo na kuwapa ahadi za uongo mara kwa mara.

Awali, akitoa taarifa za ujenzi wa Shule ya Sekondari mpya ya Kibumaye, Mkuu wa Sekondari ya Mogabiri Mwalimu Magudila Mgeta amesema Shule ya Sekondari Mogabiri ilipokea shilingi 584,280,09/= tarehe 23 Juni, 2024 kutoka mradi wa SEQUIP na ujenzi wa shule hiyo umeanza Novemba, 2024 baada ya mchakato wa kupata vifungu na manunuzi kukamilika.

Mwalimu Mgeta amesema mradi kwa sasa upo asilimia 40 ambapo madarasa nane na maabara mbili zipo katika hatua za kupauliwa, maktaba ipo hatua ya boma, maabara moja na jengo la utawala yapo hatua za msingi wakati jengo la TEHAMA lipo katika hatua ya boma.

Mwalimu Mgeta amesema mradi umechelewa kuanza utekelezaji kutokana na fedha kuingia katika mwisho wa mwaka wa fedha wa 2023/2024, kukosekana kwa vifungu na tatizo la wazabuni kushindania zabuni na kukataa kazi na fedha iliyotumika ni shilingi 74,705,260 kwa ajili ya kulipia vifaa na mafundi.

Amesema kwa sasa wanasubiria mzabuni alete mbao za kuezekea na fundi mmoja aliyepewa kazi amepata ajali wanasubiria apate nafuu aendelee na kazi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Sekondari ya Julius Kambarage Nyerere Mwalimu Melania Julius Gerald amesema Shule hiyo ilianza mwaka 2014 ikiwa na kidato cha kwanza hadi cha nne mchanganyiko na mwaka 2020 ilianza kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano wasichana.

Amesema kwa sasa Shule hiyo inawanafunzi 1056 na ina jumla ya walimu 24 na kwa sasa shule hiyo inatekeleza miradi mitano yenye thamani ya shilingi 216,400,000/= na kwa sasa ipo katika hatua mbalimbali.  

Taarifa zote mbili za miradi hiyo zilionyesha kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umechelewa kutokana na ucheleweshwaji wa vifaa kutoka kwa mzabuni aliyefahamika kama Mama Leah aliyeshinda zabuni ya usambazaji wa vifaa katika miradi hiyo.

Katika ziara hiyo Mhe. Mtambi aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, baadhi ya Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na wazabuni na mafundi wanaotekeleza mradi huo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.