• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RCC yapitisha bajeti ya zaidi ya bilioni 356

Posted on: March 6th, 2024

Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara leo imepitisha mapendekezo ya mpango na bajeti ya Mkoa wa Mara kwa mwaka wa fedha 2024/2025 yenye jumla ya shilingi 356,879,507,000 kwa ajili ya mishahara miradi ya maendeleo na matumizi menginey.

Akiwasilisha mpango na Bajeti katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mpango na Uratibu Bwana Emmanuel Mazengo amesema kiasi hicho ni ongezeko la asilimia 13 ukilinganisha na kiasi cha shilingi 317,045,656,000 kilichoidhinishwa mwaka wa fedha 2023/2024.

“Fedha zinazoombwa zinajumuisha shilingi 263.053,556,000 za matumizi ya kawaida na shilingi 93,825,951,000 za shughuli za maendeleo” amesema Bwana Mazengo.  

Bwana Mazengo ameeleza kuwa kati ya fedha hizo shilingi bilioni 10,328,357,000 ni kwa ajili ya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wakati shilingi 346,551,043,000 ni bajeti ya jumla ya Halmashauri tisa za Mkoa wa Mara.

Bwana Mazengo amevitaja vipaumbele vya bajeti katika mwaka wa fedha 2024/2025 ni pamoja na kuendelea na uboreshaji wa sekta ya elimu; kuendelea na uboreshaji wa sekta ya afya; huduma za utawala na uchumi na uzalishaji mali.

Kikao hicho pia kimepokea na kujadili mapendekezo ya mpango wa bajeti ya maendeleo ya sekta ya maji; mapendekezo na mpango wa bajeti ya sekta ya nishati (TANESCO); taarifa kuhusu mitambo ya uchimbaji wa visima vya maji na uchorongaji madini iliyopokelewa katika Mkoa wa Mara.

Mambo mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na maombi ya vijana wanaoshiriki mradi wa BBT kupatiwa eneo la kilimo na maombi ya kuigawanya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ili  kuwasaidia wananchi kupata huduma kiurahisi.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda kimeridhia masuala yote isipokuwa suala la mgawanyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambalo kikao kimeliacha kwa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara kulifanyiakazi suala hilo.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na viongozi wa vyama vya siasa, wabunge wa Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Meya na wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, viongozi wa dini na waalikwa wengine.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.