• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC Mtambi aongoza waombolezaji mazishi ya Meja Jenerali Charles Mbuge

Posted on: October 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amewaongoza viongozi, wananchi na waombolezaji katika mazishi ya Meja Jenerali Mstaafu Charles Mang’ere Mbuge aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera na Mratibu wa Idara ya Majanga na Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Mtambi ametoa pole kwa wafiwa, ndugu, jamaa na waombolezaji wote na kuwataka waombolezaji hao kutafakari kuhusu safari yao ya maisha hapa duniani.

“Maisha ni siku tatu: jana, leo na kesho, jana huijui leo tunayo, kesho huijui, kumbe sote tutaenda njia hii aliyotangulia mwenzetu na suala la msingi la kujiuliza tunaendaje? Mwenzetu kaenda vizuri, sisi tutaendaje?” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa kawaida watu huwa wanafariki mwezi mmoja kabla, mwezi waliozaliwa au mwezi mmoja baada ya mwezi wa kuzaliwa na Meja Jenerali Mbuge alizaliwa tarehe 06 Oktoba, 1963 na amefariki tarehe 12 Oktoba, 2024.

“Ni imani yangu kuwa wakati wake ulikuwa umefika na amepumzika, na amepumzika kupumzika ambako wengine tunasema kumetukuka…. Amepumzika vizuri kweli kweli kazi kwetu sisi ambao bado tuna uhai tujitafakari maisha yetu” amesema Mhe. Mtambi.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Mtambi amesema marehemu kama wazungumzaji wengi walivyosema alikuwa mchapakazi sana kama ilivyo sifa ya wananchi wa Mkoa wa Mara na kuongeza kuwa wanamara ni wachapakazi sana.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa wa Kanda ya Ziwa Mhe. Mtambi amesema marehemu alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, moja ya mikoa ya Kanda ya Ziwa na katika mazishi hayo kuna uwakilishi kutoka mikoa yote ya Kanda ya Ziwa na wanayo rambirambi yao ambayo wataiwasilisha kwenye familia ya marehemu.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi na waombolezaji kujiandikisha katika daftari la mkaazi wa Mtaa/Kijiji zoezi linaloendelea kitaifa hadi tarehe 20 Oktoba, 2024 ili waweze kushiriki kupiga kuwa katika uchaguzi Serikali za Mitaa utakaofanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024.

Taarifa ya wasifu wa marehemu inaonyesha kuwa alizaliwa tarehe 06 Oktoba, 2024 katika Kijiji cha Nyamongo, Kata ya Kukilango Tarafa ya Makongoro, Wilaya ya Butiama na amefariki tarehe 12 Oktoba, 2024 katika Hospitali ya Appolo nchini India na baadaye kurudishwa nchini tarehe 14 Oktoba, 2024.

Meja Jenerali Mbuge amesoma Shule ya Msingi Lugalo mwaka 1974-1980 na Shule ya Sekondari Kigurunyembe mwaka 1981-1984 na baadaye akajiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) tarehe 01 Januari, 1985 na amelitumikia jeshi kwa muda wa miaka 38, miezi saba na siku nne.  

Mhe. Mbuge alihudhuria kozi mbalimbali ikiwemo kozi ya Afisa Mwanafunzi nchini Tanznaia na kutunukiwa Kamisheni tarehe 28 Machi, 1991 na alipandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali hadi cheo cha Meja Jenerali tarehe 02 Juni, 2020.

Meja Jenerali Mstaafu Mbuge amewahi kushika madaraka mbalimbali ikiwemo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mwaka 2019-2021, Mkuu wa Mkoa wa Kagera mwaka 2021-2022 na Mratibu wa Idara ya Majanga na Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu kuanzia mwaka 2022 hadi alipostaafu jeshini kwa heshima tarehe 05 Oktoba, 2023.

Viongozi na waombolezaji mbalimbali waliopata nafasi ya kutoa salamu wamemzungumzia Meja Jenerali Mstaafu Mbuge kuwa alikuwa mchapakazi na aliyetekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa na muasisi wa neno HAPA KAZI TU!.

Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mohamed Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenan Kihongosi, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mhe. Patrick Chandi Marwa, Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Venance Salvatory Mabeyo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini.

Wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi, Meja Jenerali Rajabu Mabele, viongozi mbalimbali wa Jeshi, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara na Wilaya ya Butiama, Wakuu wa Wilaya mbalimbali wa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.