• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC Mara awataka wananchi kuchukua tahadhari ya MURBUG

Posted on: January 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao utambulisho wa kazi na majukumu ya Mamlaka ya Kudhibiti Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuchukua tahadhari na kujilinda dhidi ya tishio la kusambaa kwa maabukizi ya ugonjwa wa murbug hapa nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amesema japokuwa kwa sasa tishio la ugonjwa huo sio kubwa lakini wananchi wachukue tahadhari kwa kuwa ugonjwa huo hauna kinga wala tiba na unasababisha vifo kwa asilimia zaidi ya 80 ya wagonjwa wanaopata maambuki ya ugonjwa huo.

“Japokuwa kwa sasa ni mtu mmoja amegundulika katika Mkoa wa Kagera, lakini bado kuna uwezekano wa uwepo wa wagonjwa wengine ambao bado hawajagundulika au huyo mgonjwa anaweza kuwa ameshawaambukiza watu wengine kabla yeye hajagundulika” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuwasikiliza na kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya kuhusiana na namna ya kukabiliana na tishio la ugonjwa huo na hususan kuacha baadhi ya tabia za mazoea zilizozoeleka katika jamii na kuanza tena utaratibu wa kunawa mikono maji tiririka na sabuni kila wakati.

Mhe. Mtambi amewataka wataalamu wa afya, Wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri kuendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na kutoa miongozo ya namna ya kukabiliana na tishio la kuenea kwa ugonjwa huo hapa nchini.  

Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe, Ustawi wa Jamii Bwana Erick Yossam Muhigi amesema amesema Mkoa wa Mara unaendelea na utoaji wa Elimu kwa wananchi kuhusiana na ugonjwa wa Murbug na hususan baada ya kugundulika mgonjwa mmoja katika Mkoa wa Kagera.

Bwana Muhigi amezitaja dalili za ugonjwa wa murbug kuwa ni pamoja na muathirika kupata homa kali, kuharisha, kuharisha damu, kutapika, kutapika damu na kutokwa na damu katika sehemu mbalimbali mwilini.

“Ugonjwa huu unaenea kwa njia mbalimbali ikiwemo kugusa jasho, mkojo, damu, kinyesi, matapishi, nguo, matandiko, kugusana na mtu aliyeathrika na ugonjwa huo au wanyama walioathirika na ugonjwa huo” amesema Bwana Muhigi.

Bwana Muhigi amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kunawa maji tiririka na sabuni, kuepuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyoathirika na ugonjwa huo na kuepuka kula mizoga ya wanyama waliokufa kutokana na uwezekano wa kula nyama ya mnyama aliyeathrika na ugonjwa huo.

Bwana Muhigi amesema ugonjwa huu unasambaa kwa haraka katika jamii na mtu ambaye ameathirika na ugonjwa huu anaanza kuonyesha dalili za kuwa na ugonjwa wa murbug baada ya siku mbili hadi 21 na muathirika huyo anaweza kuwaambukiza wengine hata kama hana dalili za ugonjwa huo jambo ambalo linaongeza kusambaa kwa maambukizi katika jamii.

Bwana Muhigi amesema Mkoa wa Mara umeimarisha udhibiti wa wagonjwa katika mpaka wa Sirari na vivuko vya wananchi kupita kutoka nchi jirani, udhibiti wa Uwanja wa Ndege wa Musoma na viwanja vigine vya ndege vilivyoko katika Mkoa wa Mara.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama Mkoa, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, maafisa kutoka taasisi mbalimbali, Halmashauri za Mkoa wa Mara, wadau wa kilimo, mifugo na biashara Mkoa wa Mara.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.