• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC Mara ampongeza mwekezaji wa Mara Mining Investment

Posted on: September 13th, 2022

RC AMPONGEZA MWEKEZAJI MARA MINING INVESTMENT

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo ametembelea Mgodi wa Dhahabu wa Mara Miningi Investment katika Kijiji cha Kerende, eneo la Nyamongo katika Wilaya ya Tarime na kumpongeza mmiliki wa mgodi huo kwa kufanya uwekezaji mkubwa.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua migodi katika mgodi huo, Mheshimiwa Mzee amempongeza mmiliki wa mgodi huo kwa uthubutu katika uwekezaji.

“Ninakupongeza sana kwa uwekezaji unaoufanya na kuweza kutoa kodi kwa serikali na ajira kwa watanzania na maendeleo katika eneo hili” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, akiwa katika eneo hilo Mkuu wa Mkoa alipokea taarifa za maendeleo ya mgodi huo na kukagua shughuli za mgodi.   

Akitoa taarifa ya mgodi huo, Mkurugenzi Mkuu wa mgodi huo Bwana Josephat Muniko Mwita ameeleza kuwa uchimbaji wa madini katika mgodi huo ulianza tangu mwaka 1937 na umekuwa ukifanywa na wamiliki tofauti watano.

Bwana Mwita ameeleza kuwa aliununua mgodi huo baada ya kupata ruzuku kutoka serikalini mwaka 2007 na tangia hapo amekuwa akiendelea na shughuli za uchimbaji mpaka sasa

Bwana Mwita ameeleza kuwa kwa sasa mgodi huo umeajiri wafanyakazi 150 wenye ajira za kudumu na ajira za muda na ameshachangia pato la taifa zaidi ya shilingi milioni 500 kama kodi na ushuru wa huduma na kupanda miti 10,000 katika eneo la mgodi huo.

Aidha, Bwana Mwita ambaye pia ni mmiliki wa mgodi huo ameeleza kuwa mgodi huo umekuwa ukipokea wanafunzi wanaofanya mafunzo kwa vitendo ya uchimbaji madini kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini.

Bwana Mwita ameeleza kuwa pamoja na mafanikio mbalimbali waliyoyapata mgodi huo unakabiliwa na changamoto ya mtaji wa kupanua zaidi shughuli zao, wananchi kutegesha karibu na eneo la mgodi ili walipwe fidia na gharama kubwa za kukodi vifaa vya utafiti. 

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mara aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara na maafisa wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara.   

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.