• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC Azitaka Halmashauri kubuni vyanzo vya mapato

Posted on: January 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Mara kubuni vyanzo vipya na endelevu vya mapato ili kuweza kuboresha makusanyo ya Halmashauri hizo na huduma kwa wananchi.

Akizungumza leo katika kikao cha tathmini ya utendaji kazi Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji, Mhe. Mtanda amezipongeza Halmashauri zilizofanya vizuri katika makusanyo ya robo ya kwanza na robo ya pili ya mwaka wa Fedha 2023/2024.

“Bila kuwa na mapato ya kutosha na endelevu, Halmashauri hazitaweza kutekeleza majukumu yake na hivyo kushindwa kujiendesha katika masuala ya msingi ya kuwahudumia wananchi kutokana na ukosefu wa fedha” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amezitaka Halmashauri kuacha kutegemea vyanzo vya mapato ambavyo havina tija tena kama vile uvuvi na kilimo ambavyo kwa muda mrefu vimekuwa havifanyi vizuri lakini ndio vyanzo vikuu vya mapato kwa baadhi ya Halmashauri.

Mhe. Mtanda amezishauri Halmashauri kuwekeza katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ili kuwezesha wananchi kuzalisha samaki kwa wingi na hivyo kuongeza samaki katika Ziwa Victoria na hatimaye kuongeza mapato ya Halmashauri.  

Amewataka Wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri kutoa msukumo zaidi katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kuwataka Maafisa Mipango wa Halmashauri kufanya ushirikishaji wa kutosha katika kubuni mipango ya Halmashauri zao.

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri kuwafuatilia kwa ukaribu wakusanya mapato na kuhakikisha kuwa wanakusanya kupitia mfumo na wanaweka fedha benki kwa wakati kwa mujibu wa makubaliano ya mikataba yao.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashauri zote kuhakikisha kuwa watoto wote  waliopaswa kuanza darasa la awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza wanaenda shule na kuanza masomo kabla ya tarehe 31 Marchi, 2024.

Amewataka Wakuu wa Divisheni za Elimu kwa kushirikiana na viongozi na watendaji mbalimbali kufanya msako wa nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha watoto wote wanaenda shule kuanza masomo yao kwa mwaka 2024.

Awali akitoa taarifa ya uandikishaji, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Bulenga Makwasa amesema kwa sasa masomo yameshaanza japokuwa muda wa kupokea watoto bado upo hadi tarehe 31 Machi, 2024.

 Bwana Makwasa amewaomba viongozi kushirikiana ili kuwawezesha watoto wengi zaidi kuanza masomo na kunufaika na elimu bure inayotolewa kuanzia madarasa ya awali hadi Kidato cha Sita hapa nchini.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.