• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC azindua mradi wa Utafiti unaofadhiliwa na IRDC

Posted on: November 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amezindua mradi wa utafiti wa “Kuhamasisha Uanzishaji wa Ajira na Miradi ya Kiuchumi kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu” unaofadhiliwa na Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Maendeleo (IRDC) cha Canada.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Mzee amewataka watafiti hao kuhakikisha wanaufanya utafiti huo na kutoa matokeo ya utafiti huo kwa haraka ili Serikali ikiyafanyia kazi mapungufu yaliyopo iweze kuwasaidia wananchi.

“Matokeo ya utafiti huu tunatarajia yapunguze athari za mapungufu yanayoendelea kwa sasa katika utoaji wa mikopo ya makundi maalum kwa Halmashauri zetu, sasa yakichelewa sana hayatakuwa na manufaa tunayoyatarajia” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, ametoa changamoto kwa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia kuhakikisha wasomi watakaopita katika Chuo hicho wanajiajiri na wanaajiri wengine ili kupunguza uhaba wa ajira hapa nchini.

Kwa upande wake Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) Prof. Lesakit Mellau ameeleza kuwa mradi huo utafanyika katika kipindi cha miaka mitatu na gharama ya mradi mzima ni shilingi milioni 910.

Prof.Mellau ameeleza kuwa mradi huo unaunganisha mafunzo kwa wahadhiri watatu mmoja katika Shahada ya Uzamivu na wawili katika Shahada ya Uzamili pamoja na utafiti utakaofanyika katika Mikoa ya Mara na Arusha.

Ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara utafiti utafanyika katika Halmashauri  ya Wilaya ya Butiama, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Mji wa Bunda, Manispaa ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda,  na Halmashauri tatu za Mkoa wa Arusha ambazo ni Halmashauri ya Jiji la Arusha, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Halmashauri ya Wilaya ya Longido.

Prof. Mellau ameeleza kuwa dhima ya Chuo hicho ni Pata Elimu, Jiajiri, Tengeneza Ajira ambayo inalengo la kuhamasisha wanachuo wa Chuo hicho kusoma kwa bidi ili kuja kujiajiri na kutengeneza ajira za kuajiri watu wengine.

Uzinduzi wa utafiti huo umehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, wataalamu wa Chuo hicho, Wakurugenzi wa Halmashauri zitakazopitiwa na utafiti, mashirika yasiyo ya kiserikali na watafiti watakaohusika katika Mradi huo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.