• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC awataka wafanyabiashara wa madini kufuata sheria

Posted on: October 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo tarehe 11 Septemba, 2022 amekutana na wafanya biashara wadogo wa madini katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuwataka wafanyabiashara hao kufanya biashara kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Mzee amesema ameshatembelea migodi yote ya madini katika Mkoa wa Mara na kugundua kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa madini wanafanya biashara hiyo kiujanja ujanja ili kukwepa kulipa maduhuli stahiki ya Serikali.

“Mkilipa vizuri kodi, mrahaba na ushuru wa huduma itakuwa rahisi kupata huduma za kijamii katika maeneo yenu mnapofanyia biashara ikiwa ni pamoja na barabara, hospitali, maji na shule, na mimi nitahakikisha mnapata huduma bora” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee pia amewataka wafanyabiashara wadogo wote wa madini kukata leseni halali za biashara ili kuwawezesha kuwa huru katika kufanya biashara zao.

Kwa upande wake, Bwana Jakson Ngassa ameiomba Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kuanza haraka mchakato wa kununua madini ya dhahabu ili wafanyabiashara wa madini wasiathirike na kushuka kwa bei ya dhahabu katika soko la dunia.  

“Hii itatusaidia sisi ambao hatuna mtaji mkubwa kuweza kuhimili ushindani wa kibiashara katika soko la dunia” amesema Bwana Ngassa.

Bwana Ngasa ameeleza kuwa kutoka kwenye uchimbaji soko liko vizuri, lakini katika soko la dunia bei ya dhahabu inacheza sana na wafanyabiashara wengi wanapata hasara kubwa katika hiyo bei.

Aidha, kwa upande wao wafanyabiashara kutoka Mgodi wa Irasanilo uliopo katika eneo la Buhemba, Wilaya ya Butiama wamelalamikia kukosekana kwa mahitaji muhimu katika eneo hilo hususan hospitali.

“Wachimbaji wengi wanapoteza maisha kutokana na umbali kutoka eneo la mgodi hadi ilipo hospitali, na katika uchimbaji ajali zinatokea mara kwa mara” walisema wafanyabiashara hao.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.