• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC awataka wadau kuhamasisha Sensa

Posted on: August 18th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 16 Agosti, 2022 amewataka wadau wote wa Sensa ya Watu na Makazi katika Mkoa wa Mara kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 itakayofanyika tarehe 23 Agosti, 2022.

Mheshimiwa Mzee ameitoa kauli hiyo leo katika kikao cha uhamasishaji wa sensa kwa viongozi wa dini, vyama vya siasa, Shirikisho la Wafanyabiashara, wazee wa mila na Waandishi wa Habari kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninatambua umuhimu wa kila kundi lililopo hapa, na kwa sababu suala la Sensa ni kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu, ninaomba kila mmoja wetu kwenye eneo lake atumie muda uliobakia kuwahamasisha wananchi hasa wale ambao hawajaelewa kuhusu zoezi la Sensa” alisema Mheshimiwa Mzee. 

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa wananchi wanapaswa kupewa elimu juu ya sensa ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022.  

Amewataka Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara kutumia vyombo vyao vya ndani ya Mkoa, kitaifa na kuwashirikisha waandishi wa nchi jirani kutoa  elimu ya sensa kwa wananchi wa Mkoa wa Mara ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.

Amewahamasisha wadau kuwahamasisha wananchi wote kuwatoa watu wenye ulemavu waliopo katika maeneo yao ili waweze kuhesabiwa kiurahisi. “Ukiwa na ndugu mlemavu, usimfiche, kujulikana kwake ndio itakuwa rahisi kwake kusaidiwa katika ulemavu wake” alisema Mheshimiwa Mzee.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mheshimiwa Samwel Kiboye ameeleza kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara kimekuwa kikihamasisha Sensa ya Watu, 2022 na Makazi katika maeneo mbalimbali.

Amewataka wadau walioshiriki katika kikao hicho kuacha masuala mengine yote na kuitangaza Sensa kwa muda huu uliobakia ili iweze kufanyika kwa ufanisi zaidi.

Aidha, ameahidi kutoa ushirikiano kuhakikisha zoezi la Sensa linafanikiwa na Mkoa wa Mara unafanya vizuri katika zoezi la Sensa.

 Kikao cha wadau wa Sensa kilifanyika ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 na kuhudhuriwa na wawakilishi wa makundi mbalimbali katika jamii.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.