• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC atoa miezi minne kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ndani ya miezi miwili ili iweze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo haya leo tarehe 4 Agosti 2021 wakati alipofanya ziara katika halmashauri hiyo kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

“Haiwezekani wataalamu mmekaa tu fedha inakuja mpaka inarudi bila kufanyiwa kitu chochote kile, sasa naagiza hadi kufikia mwishoni mwa Desemba 2021 hospitali hii iwe inatumika na hatutakubali tena visingizio,” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Musoma kuhakikisha ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa katika hospitali hiyo ambayo imeletewa fedha miezi sita iliyopita unaanza na unakamilika kwa haraka.

Mheshimiwa Hapi ameitaka SUMA JKT inayojenga mradi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa mkataba.

Awali wakitoa taarifa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wlaya ya Musoma Bwana Frank Magabiro pamoja na Mhandisi wa wilaya Gibai James Maige wameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo ulianza kutekelezwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Hata hivyo mradi huo haukukamilika kwa sababu fedha zake baada ya muda wa matumizi kuisha zilirudishwa serikalini, baadaye zikaletwa tena Mei, 2021 lakini hadi tarehe 30 Juni 2021 fedha hizo hazikutumika zikarudi tena serikalini.

Aidha walieleza kuwa kwa sasa fedha hizo zimeletwa tena na wapo katika mchakato wa kununua vifaa na kuleta maji eneo la ujenzi ili kukamilisha ujenzi huo.

Wakati huo huo hospitali hiyo ilipokea fedha za ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa lakini halmashauri imenunua baadhi ya vifaa vya ujenzi na kufyatua matofali lakini ujenzi haujaanza.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi pia alitembelea mradi wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Musoma, miradi ya Shule ya Sekondari ya Msihakamano, Sekondari ya Ufundi ya Musoma na Bandari ya Musoma inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Musoma na viongozi wengine.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.