• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC apokea maafisa wa Israel

Posted on: August 25th, 2022

RC APOKEA MAAFISA WA ISRAEL

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 24 Agosti, 2022 amewapokea maafisa wanne kutoka Tel Aviv Sourasky Medical Center, Lis Maternity and Women’s Hospital kutoka nchini Israel ambao wamekuja kwa ajili ya kuanzisha mradi mpya wenye lengo la kuboresha huduma za afya ya uzazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza baada ya kuwapokea maafisa hao, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa amefurahi sana kwa nchi ya Israel kuanzisha mradi wa kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na kuwaahidi wataalamu hao kuwa Mkoa wa Mara utawapa ushirikiano katika kutelekeza mradi huo.  

Katika Mapokezi hayo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, wataalamu wa afya na baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Maafisa waliopokelewa kutoka Israel ni Dkt. Gilard Rattan Moshe, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akina Mama, Binat Sessan, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Wodi ya Wazazi, Rinat Segal, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Mafunzo na Revital Levi Ari, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Mbadala wa hospitali ya Tel Aviv.  

Aidha, maafisa hao wamewasilisha nyaraka za msaada wa vifaa tiba mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Dola za Kimarekani 13,500 ambayo Serikali ya Israeli imetoa kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Wakizungumza wakati wa kupokea taarifa ya sekta ya afya ya Mkoa wa Mara, maafisa hao kutoka Israel wameahidi kuendelea kutoa msaada wa vifaa tiba na mafunzo ya muda mfupi kwa madaktari wa kawaida ili waweze kufanya vizuri operesheni za uzazi katika maeneo yao.

“Katika nchi nyingi zilizoendelea madaktari wa kawaida hawaruhusiwi kuwafanyia operesheni kwa akina mama wajawazito, lakini huku kutokana na upungufu wa madaktari bingwa, madaktari wa kawaida ambao hawana utaalamu na masuala ya uzazi wanaruhusiwa kuwafanyia upasuaji wajawazito jambo ambalo linaweza kuwa ni hatari” walisema wataalamu hao.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Dkt. Juma Mfanga amewashukuru wageni hao kwa kutaka kuanzisha mradi katika Mkoa wa Mara na kuwasilisha nyaraka za msaada huo na kuwaahidi Mkoa wa Mara utawapa ushirikiano wa kutosha katika kuimarisha ushirikiano baina ya Israeli na Tanzania.

Mbali na kuembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wataalamu hao pia wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara katika eneo la Kwangwa na vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Kabla ya kuja Mkoa wa Mara, wataalamu hao walikutana na Mganga Mkuu wa Serikali kutoka Wizara ya Afya, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya na Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.