• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC aomba jeshi kuwekeza zaidi Mara

Posted on: January 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee amemuaomba Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda kuangalia uwezekano wa Jeshi la Tanzania kuwekeza zaidi katika shughuli za uzalishaji mali katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ametoa ombi hilo wakati akimkaribisha Jenerali Mkunda aliyetembelea ofisini kwake wakati wa ziara yake ya kujitambulisha katika Vikosi vya jeshi vilivyomo katika Mkoa wa Mara na kuomba Jeshi liwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji na ufugaji waa samaki.

“Mkoa wa Mara tuna eneo kubwa linalopakana na Ziwa Victoria na mito lakini hamna kilimo cha umwagiliaji na hata ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba unafanywa kwa sehemu kubwa na jeshi tu, wananchi hawajapata elimu hiyo” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Amelipongeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kuwekeza katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba lakini ameliomba kuongeza zaidi uwekezaji na kuwafundisha wananchi wa Mkoa wa Mara kuhusiana na ufugaji wa samaki wa kitaalamu ili kuongeza uzalishaji katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa pamoja na mvua na uwepo wa Ziwa Victoria katika Mkoa wa Mara, hamna kilimo cha umwagiliaji na wakulima wengi hata wanaoishi kando kando ya ziwa wanalima kwa kutegemea mvua tu jambo ambalo alisema halileti tija.

“Hawa wananchi pamoja na elimu, lakini wanahitaji zaidi mfano waone jinsi kilimo cha umwagiliaji kinavyofayika na watapata nafasi ya kuiga jambo ambalo linaweza kukuza uchumi wao mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameliomba Jeshi kusaidia katika kukabiliana na uvamizi wa wavuvi katika Ziwa Victoria unaofanywa na wavamizi kutoka nchi Jirani za Kenya na Uganda jambo ambalo amesema linahatarisha maisha na kuwapa umaskini wavuvi wa Tanzania.  

Kwa upande wake Jenerali Mkunda ameshukuru kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na kuahidi kuangalia uwezekano wa Jeshi kuwekeza zaidi katika Mkoa wa Mara.  

Jenerali Mkunda amemtaka Mkuu wa Mkoa kumtumia Mkuu wa Brigedi ya Magharibi yenye Makao Makuu yake katika Mkoa wa Tabora kufanikisha mipango mbalimbali ya maendeleo inayohitaji kufanywa na Jeshi katika Mkoa wa Mara.

Mkuu wa Majeshi amemahidi kuwa Jeshi litaendelea kulifuatilia kwa ukaribu tatizo la uvamizi wa wavuvi katika Ziwa Victoria ili kuweza kuchukua hatua stahiki kukomesha vitendo hivyo.

Aidha, amempongeza Mheshimiwa Mzee na viongozi wote wa Mkoa wa Mara kwa jitihada zinazoendelea kuchukuliwa kukabiliana na mila potofu ya ukeketaji wa wanawake katika Mkoa wa Mara.

Hii ni mara ya kwanza Jenerali Mkunda kutembelea Mkoa wa Mara tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Juni, 2022.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.