• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC amtaka Mkandarasi kutoa maelezo

Posted on: June 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Ally Hapi ametoa saa 48 kwa mkandarasi anayejenga Uwanja wa Ndege Musoma kufika ofisini kwake kutoa maelezo kwa nini maelekezo aliyoyatoa kuhusiana na ujenzi wa uwanja huo hayajatekelezwa.

Mheshiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo katika kikao cha wakandarasi wanaotekeleza miradi yao katika Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninatoa saa 48 huyo mkandarasi afike kutoa maelezo kwa nini maelekezo niliyoyatoa mwezi Machi, 2022 hayajafanyiwa kazi mpaka sasa na mradi bado upo nyuma sana katika utekelezaji wake” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi amefikia hatua hiyo baada ya mwakilishi wa Mkandarasi huyo Beijing Construction Engineering Group (BCEG) kushindwa kutoa maelezo kwa nini maagizo ya Mkuu wa Mkoa aiyoyatoa hayajatekelezwa.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Mara akiwa ameambatana na wajumbe wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara walitembelea mradi huo tarehe 1 Machi, 2022 na kukagua maendeleo ya ujenzi pamoja na kupatiwa taarifa.

Akiwa katika mradi huo, Mkuu wa Mkoa aliwagiza mkandarasi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa mujibu wa mkataba tarehe 30 Desemba, 2022 ili ndege za abiria ziweze kuanza kutua katika uwanja huo.

Mheshimiwa Hapi alimwagiza mkandarasi kufunga taa na kufanyakazi kwa saa 24, kuongeza vifaa na watumishi katika utekelezaji wa mradi huo, hata hivyo maagizo hayo hayajatekelezwa na mwakilishi wa mkandarasi alisema haiwezekani mradi huo kukamilika kwa muda uliobakia.

Maelezo ya Meneja wa Wakala Barabara (TANROADS) ambao ndio wasimamizi wa mradi huo, kwa sasa mradi huo upo katika asilimia 18 wakati muda wa utekelezaji wa mradi umeshafika asilimia 52.

Aidha mkandarasi ameshalipwa malipo ya awali na kwa sasa hana madai ya malipo ambayo ameshayawasilisha kwa TANROADS.

Uwanja wa Ndege wa Musoma ni muhimu katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Mara na kurahisisha safari za watalii wanaoingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, kukwama kwa ukamilishaji wa uwanja huu kunaathiri uchumi wa Mkoa na wananchi wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.