• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC amkaribisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji

Posted on: July 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ofisini kwake amempokea na kuzungumza na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ambaye amefanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza baada ya kuwasili, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amempongeza Mhe. Mtambi kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuuongoza Mkoa wa Mara.

Kamishna Makakala ameeleza kuwa lengo la ziara yake katika Mkoa wa Mara ni kushughulikia maombi ya walowezi wa muda mrefu ambao walihamia kutoka nchi ya Kenya ambao wanadai vitambulisho vya uraia.

“Tunashughulikia vitambulisho hivyo ili tunapoelekea kwenye uchaguzi wale wanaostahili kupata vitambulisho hivyo wawe navyo ili iwasaidie katika kutumia haki yao ya kuchagua viongozi” amesema Dkt. Makakala.

Dkt. Makakala amesema ofisi yake inashughulikia changamoto za ofisi ya Kamanda wa Uhamiaji Mkoa wa Mara ikiwemo suala la upungufu wa watumishi na usafiri kwa maafisa wa uhamiaji.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amemshukuru Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa kufanya ziara katika Mkoa wa Mara na kumshukuru kwa ushirikiano wa ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mara kwa viongozi wa Mkoa.

Mhe. Mtambi amesema Mkoa wa Mara una waloweze wengi ambao wamekuwa wakifuatilia kadi ya mpiga kura, namba ya utambulisho wa Taifa na vitambulisho vingine vya uraia na wamekuwa wakiwatumia wanasiasa kufuatilia vitambulisho hivyo.

Mhe. Mtambi amemuomba Dkt. Makakala asiondoke kabla ya kuonja nyama choma ya Mkoa wa Mara na kutokana na mifugo yake kufugwa kwenye mazingira mazuri na kujionea utamu na ubora wa nyama choma ya Mkoa wa Mara.

“Haya mazingira inaonekana Mungu aliyaandaa kwa ajili ya wanyama na ndio maana sehemu kubw aya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ipo Mkoa wa Mara bahati mbaya wanyama hawa hawauzwi sana Tanzania wanapelekwa nchi jirani kwa njia ya magendo” amesema Mhe. Mtambi.  

Katika ziara hiyo, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji ameambatana na Maafisa mbalimbali kutoka Jeshi la Uhamiaji Makao Makuu na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mara.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.