• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC aipongeza Idara ya Afya

Posted on: August 30th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenarali Suleiman Mungiya Mzee leo ameipongeza Idara ya Afya ya Mkoa wa Mara kwa kufanikisha awamu ya pili ya chanjo ya polio kwa Watoto chini ya miaka mitano iliyofanyika hapa nchini kuanzia Mei 18-22, 2022.

Mheshimiwa Mzee ametoa pongezi hizo leo wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi Mkoa wa Mara mahususi kwa ajili ya utekelezaji wa kampeni ya chanjo ya polio yam atone kwa awamu ya tatu inayotarajiwa kuanza tarehe 1-4 Septemba, 2022.

“Katika awamu ya pili Mkoa ulichanja Watoto 630,897 ambao ni sawa na asilimia 119 ya Watoto 529,725 ya Watoto waliotarajiwa kuchanjwa katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Amewataka viongozi na watendaji wote kuongeza juhudi katika kampeni na utekelezaji wa zoezi la chanjo kwa awamu ya tatu ili Mkoa uweze kufanya vizuri zaidi katika zoezi hilo kwa kutumia fedha zilizopokelewa.

Mheshimiwa Mzee amewaagiza Wakuu wa Wilaya kusimamia awamu ya tatu ya chanjo katika Wilaya zao ili zoezi hili liweze kufanikiwa katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu y Afya Dkt. Juma Mfanga ameeleza kuwa hii ni awamu ya tatu kwa Tanzania kufanya zoezi la chanjo ya polio kwa Watoto wa chini ya miaka mitano baada ya ugonjwa huo kugundulika katika nchi ya Malawi Februari, 2022.

“Kwa awamu ya kwanza ilihusika mikoa michache iliyopo jirani na nchi ya Malawi na awamu ya pili ilikuwa nchi nzima na sasa inafanyika tena nchi nzima kwa watoto wote chini ya miaka mitano” alisema Dkt. Mfanga.

Dkt. Mfanga amewataka wajumbe wa kikao hicho kutoa elimu na kuwahamasisha wananchi waweze kulipokea zoezi hilo vizuri na kutoa ushirikiano kwa maafisa wa chanjo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Mara Bibi Flowina Muuzaje ameeleza kuwa Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) watafanya kampeni ya siku nne.

Bibi Muuzaje ameeleza kuwa katika kipindi hicho kampeni itafanyika nyumba kwa nyumba na katika maeneo yote yenye watoto wa chini ya miaka mitano ikiwemo vituo vya kutolea huduma za afya kama ilivyofanyika wakati wa awamu ya pili.

Aidha Bibi Muuzaje ameeleza kuwa Mkoa bado unaendelea kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari, mikutano ya wananchi, matangazo, vipeperushi na mitandao ya kijamii.

Kikao cha Afya ya Msingi Mkoa wa Mara kilihudhuriwa pia na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Halmashauri pamoja na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.