• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RC aihakikishia Ushirikiano CCM Mara

Posted on: August 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo ameanza ziara ya kikazi katika Wilaya ya Musoma na Wilaya ya Butiama kwa kutembelea ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara kwa lengo la kujitambulisha.

Akizungumza baada ya kujitambulisha na kukaribishwa, Mkuu wa Mkoa amewaahidi ushirikiano yeye mwenyewe na viongozi wote wa serikali wa Mkoa wa Mara.

“Mimi ninawaahidi tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa Chama cha Mapinduzi na viongozi wa Chama na niwaombe ushirikiano katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa wananchi” ameeleza Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa anaamini katika mabadiliko ya kimaendeleo na ubunifu kwa ajili ya kuutoa Mkoa wa Mara sehemu ilipofikia kwenda katika maendeleo zaidi.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Mara Bwana Lengaeli Akyoo amemkaribisha Mkuu wa Mkoa na kusema kuwa watu wa Mkoa wa Mara wamefurahia uteuzi wao na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi hao.

Aidha, amewapongeza kwa kuaminiwa na kuteuliwa na Mheshimiwa Rais na kuwakaribisha Mkoa wa Mara na hususan katika Chama cha Mapinduzi.

katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu ambaye pia amewasili Mkoa wa Mara tarehe 5 Agosti, 2022 baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 28 Julai, 2022.

 Hii ni ziara ya kwanza ya Mheshimiwa Mzee katika Mkoa wa Mara baada ya kuwasili tarehe 6 Agosti, 2022 baada ya kuteuliwa na Rais tarehe 31 Julai, 2022 kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.