• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RAS Kusaya aahidi maboresho Shule ya Msingi Radienya

Posted on: January 21st, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo amefanya ziara katika Wilaya ya Rorya na kutembelea Shule ya Msingi Radienya iliyoko katika Kata ya Kirogo na kuahidi maboresho makubwa katika miundombinu na idadi ya walimu wa shule hiyo.

“Shule hii tutaifanyia maboresho makubwa hivi karibuni na hususan miundombinu ili mazingira yawe rafiki kwa walimu na wanafunzi na kuongeza idadi ya walimu wanaofundisha katika shule hii” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amemuagiza Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kufuatilia kwa ukaribu maboresho yanayohitajika katika shule hiyo ili kuwashirikisha wadau wa elimu na kuzitumia vizuri fursa zinazotolewa na Serikali katika uboreshaji wa miundombinu ya shule.

Aidha, Bwana Kusaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Bwana Abdul Mtaka kutembelea shule hiyo na kuwasilisha mahitaji halisi ya shule hiyo ofisini kwake na hatua ambazo Halmashauri hiyo itazichukua kwa haraka ili shule hiyo iendelee kutumika wakati fedha za ujenzi wa shule mpya zinatafutwa.

Aidha, RAS amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Mara kuitembelea shule hiyo na kujenga barabara na daraja kuweza kupitisha magari na wanafunzi kuingia na kutoka katika shule hiyo.

Bwana Kusaya amewapongeza walimu wanaofundisha katika shule hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuwaahidi kuwaboreshea mazingira ya kufundishia na kujifunzia na nyumba za kuishi haraka iwezekanavyo.

Akiwa katika shule hiyo, Bwana kusaya amezungumza na walimu na wanafunzi, amekagua madarasa, vyoo, ofisi za walimu na nyumba za walimu na kujionea uchakavu wa miundombinu ya shule hiyo ya zamani.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Makwasa Bulenga amesema tayari Idara ya Elimu ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imewahamishia walimu wawili wengine katika shule hiyo na barua za uhamisho zipo tayari na wanatarajiwa kuwasili shuleni hapo baada ya muda mfupi.  

Bwana Bulenga amewataka walimu kujaza taarifa sahihi za hali halisi ya shule zao kwenye mfumo wa taarifa za shule hapa nchini ili kuweza kupunguza tatizo la uchakavu wa miundombinu ya shule.

“Ukiingia kwenye mfumo, shule hii inaonyesha mambo yake yapo safi, ina vyoo, madarasa ya kutosha na nyumba za walimu, lakini ukija hapa kuona hali halisi kuna darasa moja tu ndio zima majengo mengine yote ni mabovu” amesema Bwana Bulenga.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Rwehumbiza Tresphory Tryphone amesema Shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 609 wa madarasa ya awali hadi darasa la saba na walimu watano ambapo mmoja kati yao yupo masomoni na kubakiwa na walimu wanne.

Bwana Tryphone amesema shule hiyo ina vyumba saba vya madarasa ambavyo vyote ni vibovu isipokuwa chumba kimoja kilichojengwa kwa nguvu ya wananchi na kukamilishwa na Serikali ndio kina hali nzuri na shule ina matundu manne tu ya vyoo ambayo yapo katika hali mbaya.

Aidha, Mwalimu Tryphone amesema Shule hiyo inazo nyumba sita za walimu lakini mbili ni mbovu sana haziwezi kukalika na nyumba nyingine nne ni chakavu lakini bado zinaendelea kutumiwa na walimu wa shule hiyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Radienya Bwana Stephen Nyakitita amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa kwa kuitembelea shule hiyo na kuahidi kuwa viongozi wa Kijiji hicho wataendelea kuwahamasisha wananchi kusaidia katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo.

Bwana Nyakitita ameyataja matatizo makubwa ya shule hiyo kuwa ni barabara ya kuingia shuleni hapo kutokana na uwepo wa korongo kubwa sana ambalo linahatarisha maisha ya wanafunzi wanaotokea upande mmoja wa kijiji hicho wakati wa mvua.

Aidha, Bwana Nyakitita amesema wakati wa mvua magari hayawezi kuingia katika Shule hiyo kutokana na njia zote za kuingia katika shule hiyo kuwa mbaya na kulazimisha vifaa kubebwa kichwani kwa zaidi ya kilomita moja ili kuweza kuingia shuleni hayo.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Kata wa Kata ya Kirogo Bwana Justine Masau amesema miundombinu ya shule nyingi za kata hiyo ni mibovu sana na ina walimu wachache jambo ambalo liliifanya Kata hiyo kuwa ya mwisho katika mitihani yote ya shule za msingi.

Bwana Masau amesema hata hivyo alikutana na walimu wa shule za Kata hiyo na kupanga nao na mwaka 2023 kata hiyo ilitoka nafasi ya 26 hadi nafasi ya 10 na mwaka 2024 imeshika nafasi ya 12 katika matokeo ya Darasana la Saba.

Bwana Masau amemuomba Katibu Tawala kuwaongeza walimu na kuboresha miundombinu ya shule hizo ili kutoa mazingira bora ya kujifunza na kufundishia.  

 Katika ziara hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara aliambatana na baadhi ya Maafisa kutoka ofisini kwake na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.