• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RAS awataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watafiti

Posted on: December 19th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo tarehe 9 Desemba, 2023 ametoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu utafiti unaoendelea katika Mkoa wa Mara wa kukusanya taarifa za shughuli za Kijamii na Kiuchumi wa mwaka 2023/24 unaofanywa na Serikali katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

“Niwaombe wananchi wote wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa utafiti unaoendelea ili Serikali iweze kupata taarifa sahihi zitakazoiwezesha Serikali kupata taarifa sahihi kwa ajili ya kufanya maamuzi na kutunga sera sahihi kwa maendeleo ya nchi yetu” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu ameeleza kuwa utafiti huo unafanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Biashara na Viwanda na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na unafanyika katika mikoa yote kwa siku 90 kuanzia tarehe 6 Desemba, 2023.

“Taarifa za takwimu zinazokusanywa ni siri kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu sura ya 351 na zinatumika kwa malengo mahususi ikiwa ni pamoja na maandalizi ya sera na kufanya maamuzi kwa maendeleo ya Taifa” amesema Bwana Makungu.  

Kwa mujibu wa Bwana Makungu, matokeo ya utafiti huu yatawezesha kufanyika kwa uchambuzi wa kina wa hali ya kiuchumi, kupima tija katika uzalishaji na kufanya tathmini ya mwenendo wa uchumi  wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Baadhi ya maswali yatakayoulizwa na wadadisi wa utafiti huo ni pamoja na jina la shughuli, mahali ilipo, anuani ya posta, namna za simu, uhalali wa umiliki, mwaka shughuli ilipoanza kufanya kazi, usajiri wa shughuli husika, idadi ya watumishi, jumla ya mapato kwa mwaka.

Bwana Makungu ameeleza kuwa utafiti huu utafanyika kwa kuwatumia wadadisi kwenye maeneo ya vijijini na mijini ambao watakuwa na vitambulisho vya Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.