• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

RAS aongoza makabidhiano ya magari yaliyotolewa na Amref

Posted on: March 5th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara leo tarehe 05 Machi, 2025 ameongoza hafla ya kukabidhi magari matatu yaliyotolewa na Shirika llisilo la kiserikali la Amref kwa ajili ya kusaidia shughuli za usimamizi wa sekta ya afya katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi magari hayo, Bwana kusaya amewataka maafisa wanaokabidhiwa magari hayo kuyatumia vizuri kwenye shughuli za usimamizi wa sekta ya afya zilizokusudiwa na Shirika la Amref.

“Mimi nitafuatilia kwa karibu matumizi ya magari haya ili yatumike kwa makusudio yaliyopangwa ikiwa ni pamoja na kufuatilia muda wa matengenezo” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada wa magari hayo na ni nyenzo muhimu katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na kuahidi kuwa magari haya tutayatunza ili yaendelee kutoa huduma.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Dkt. Zabroni Masatu amesema kuwa magari yaliyopokelewa ni Nissan Patrol moja kwa ajili ya matumizi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na magari mawili Toyota hardtop ambayo yamekabidhiwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Dkt. Masatu amelishukuru Shirika la Amref kwa msaada huo na kusema kuwa mahitaji ya magari ya usimamizi wa shughuli mbalimbali ya sekta za afya ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa miradi ya sekta hiyo na vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mkoa wa Mara Dkt. Revocatus Masanja amesema Amref imetoa magari matatu yaliyokuwa yanatumika kwa ajili ya usimamizi wa mradi wa ukimwi katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutokana na shirika hilo kuona mahitaji.

“Magari haya bado ni mazima yakitumika vizuri yatasaidia kutatua uhaba wa changamoto za magari kwa ajili ya usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya na miradi ya sekta ya afya” amesema Dkt. Masanja.

Dkt. Masanja ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa ambao umekuwa ukitoa kwa wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Amref na kuupongeza Mkoa kwa kujali afya za wananchi wake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Bwana Msongera Palera amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada huo ambao utatatua upunguvu mkubwa wa magari katika Halmashauri hiyo.

“Awali tulikuwa tunaazima magari Amref mara kwa mara na sasa wameona watupatie gari moja iwe ya kwetu ili tuweze kuwahudumia wananchi vizuri zaidi” amesema Bwana Palera.

Bwana Palera amesema Halmashauri yao ina eneo kubwa sana na inavituo vingi vya kutolea huduma za afya kwenye vimesambaa maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo na inakuwa vigumu kwa wasimamizi wa sekta ya afya kama hawana usafiri wa uhakika.

Hafla ya mapokezi ya magari hayo imehudhuriwa na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Divisheni za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Halmashauri hizo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.