• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Ongezeni Mikopo kwa Wakulima- Samia

Posted on: August 2nd, 2020

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amezitaka taasisi za fedha kuongeza mikopo kwa kwa wakulima ili kuboresha uzalishaji wa wakulima hapa nchini.

Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameeleza hayo wakati wa hotuba yake ya uzinduzi wa maonyesho ya sikikuu ya wakulima (NANENANE) ambayo kitaifa imefanyika katika viwanja vya Nyakabindi, Mkoani Simiyu.

“Mikopo itawasaidia wakulima wetu hapa nchini kuongeza tija katika shughuli zao na hivyo kuongeza kipato cha wakulima na taifa kwa ujumla” alisema Mheshimiwa Samia.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Samia kwa sasa taasisi za fedha zinatoa mikopo kwa wakulima kwa asilimia tisa tu jambo ambalo limepelekea kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa mikopo kwa wakulima hapa nchini.  

Aidha Mheshimiwa Samia amesema serikali imesimamia uimarishaji wa mnyororo wa thamani ili kuongeza tija kwa wakulima wote hapa nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameishukuru sana serikali kwa kukubali maonyesho haya kufanyika katika Kanda ya Ziwa Mashariki kwa miaka mitatu mfululizo.

“Tunaishukuru sana serikali kwa kukubali kufanya maonyesho haya katika viwanja hivi kwa miaka mitatu mfululizo na yamekuwa na hamasa kwa wakulima wetu hapa nchini” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa imejipanga kubadili shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi ili kuongeza tija zaidi kwa wananchi wanaojihusisha na shughuli hizo.

Maonyesho ya 28 ya sherehe za wakulima (NANENANE) yamezinduliwa leo tarehe 1 Agosti 2020 na yanatarajiwa kufungwa rasmi tarehe 8 Agosti 2020 Kauli mbiu ya maonyesho ya NANENANE mwaka huu ni kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua kiongozi Bora 2020.

Kwa upande wa maonyesho ya viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu yameandaliwa na Kanda ya Ziwa Mashariki ambayo inahusisha mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.