• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Naibu Waziri Mkuu kuongoza Mazishi ya Mtendaji Mkuu TANESCO

Posted on: April 15th, 2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko anategemewa kuwaongoza waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga yatakayofanyika tarehe 16 Aprili, 2025 katika eneo la Mikungani, Wilaya ya Bunda.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhani msiba wa Mhandisi Nyamohanga, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amesema marehemu NyamoHanga alikuwa mzalendo na mpenda maendeleo ya nchi na kifo chake ni msiba mkubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na Watanzania.  

“Mhandisi Nyamohanga alikuwa mdau mkubwa wa maendeleo wa Mkoa wa Mara na ametusaidia sana katika kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kusambaza umeme katika vitongoji vya Mkoa wa Mara na maeneo ya wachimbaji wadogo wadogo ambayo awali yalikuwa hayapati umeme.

Mhe. Mtambi amesema Mhandisi amesaidia pia kupeleka umeme katika Shule ya Amali ya Mkoa inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Butiama na amesaidia pia kurejesha umeme kwa haraka wakati wa maafa yaliyosababishwa na mvua ya upepo yaliyotokea Manispaa ya Musoma kwa kuhakikisha TANESCO inarejesha umeme eneo lililoathirika haraka.  

Mhe. Mtambi ametoa pole kwa viongozi na watendaji wa Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Wizara ya Nishati, TANESCO na wafiwa wote wanaohusika katika msiba huo na kuwataka waombolezaji kuendelea kumuenzi Mhandisi Nyamohanga kwa kutenda mambo mazuri kwa Taifa letu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Ziwa wa TANESCO Mhandisi Satco Nombo amesema kwa sasa maandalizi muhimu kwa ajili ya mazishi ya Mhandisi Nyamohanga katika eneo la Migungani, Wilaya ya Bunda yanaendelea vizuri.

Mhandisi Nyamohanga amesema viongozi, menejimenti na watumishi kutoka TANESCO na Wizara ya Nishati, taasisi nyingine za Serikali na wanafamilia wanaotarajiwa kushiriki mazishi hayo wanatarajiwa kufika Bunda kuanzia tarehe 15 Aprili, 2025.

Mhandisi Nombo amesema aliyekuwa Dereva wake ambaye pia alifariki katika ajali hiyo Ndugu Mujahir Mohamed Haule tayari amesafirishwa kwenda Mkoa wa Pwani na amezikwa tarehe 14 Aprili, 2025.

Mhandisi Nyamohanga na dereva wake walifariki katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 13 Aprili, 2025 katika Kata ya Nyatwali, jirani na geti kuu la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti lililopo eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usala ya Wilaya ya Bunda, baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.