• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mzee awataka walimu kuwa wabunifu

Posted on: January 6th, 2023

MZEE AWATAKA WALIMU KUWA WABUNIFU

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewataka walimu wa shule mbalimbali katika Mkoa wa Mara kuwa wabunifu na kujiongeza katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mheshimiwa Mzee ametoa wito huo wakati akifanya ziara ya kupokea vyumba vya madarasa katika Wilaya ya Serengeti na kuwaelekeza walimu kuanzisha miradi mbalimbali ya kuongeza mapato ya shule ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

“Walimu wetu hawana ubunifu, wa kujiongezea au kufanya mabadiliko katika shule zetu, Shule zinaweza kufanya biashara ndogo ndogo na kupata pesa za kuweza kutatua changamoto ndogo ndogo zinazowakabili” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa miradi itakayoanzishwa inaweza kutoa huduma na elimu kwa vitendo kwa walimu na wanafunzi wanaosoma katika shule hizo na wananchi wanaowazunguka maeneo ya shule.  

Aidha, amewataka walimu kutumia fursa ya kuwa na wanafunzi wengi kubuni miradi ambayo itawasaidia kupata fedha za kutatua changamoto mbalimbali pindi zinapojitokeza.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka walimu na wasimamizi wa elimu kusimamia suala la uboreshaji wa mazingira ya shule kwa kupanda miti, maua, matunda na kuyasawazisha maeneo ya shule na kuzuia mmomonyoko wa udongo katika shule zao ili wanafunzi waweze kupita vizuri.

“Mazingira yanatakiwa yawe mazuri ili wanafunzi wapende kwenda shule na wakienda wajifunze kitu kutokana na ubunifu katika kuongeza mapato na kutunza mazingira” alisema Mheshimiwa Mzee.   

Katika ziara hiyo, kati ya shule tano alizotembelea, Shule ya Sekondari Rigicha pekee ilitoa taarifa ya kuwa na mradi wa shule wa ufugaji wa nyuki, lakini shule nyingine zilitoa taarifa ya kuwa na mpango wa kuanzisha miradi lakini bado hawajapata mtaji wa biashara.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Katibu Tawala sehemu ya Elimu, Katibu Tawala sehemu ya Miundombinu, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, watumishi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Menejimenti ya Wilaya ya Serengeti na viongozi wa CCM Wilaya ya Serengeti.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.