• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mwenge wa Uhuru wawasha Mwenge wa Mwitongo Butiama

Posted on: June 26th, 2021

Mwenge wa Uhuru unaoendelea na mbio zake katika Mkoa wa Mara umefika nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuwasha mwenge wa asili unaofahamika kama Mwenge wa Mwitongo.

Mwenge wa Mwitongo umewashwa leo tarehe 26 Juni 2021 ikiwa ni sehemu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambapo kila mwaka Mwenge wa Uhuru hupita nyumbani kwa Baba wa Taifa na kuwasha Mwenge wa Mwitongo kama kumbukumbu ya muasisi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa.

“Mwenge huu umekuwa ukiwashwa miaka yote tangu Baba wa Taifa akiwa hai kila Mwenge wa Uhuru unapofika katika Mkoa wa Mara, ni tukio zuri kwa kweli kulishuhudia” alisema mwananchi baada ya kuwashwa kwa mwenge huo.

Baada ya kuwasha Mwenge wa Mwitongo, viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa walipata nafasi ya kusalimiana na familia ya Nyerere iliyoongozwa na Chifu Japhet Wanzagi Nyerere akiambatana na Mtoto wa Baba wa Taifa Bwana Madaraka Nyerere na wanafamilia wengine.

Aidha viongozi hao walitumia fursa hiyo kuzuru kaburi la Mwalimu Nyerere na wakiwa hapo waliweka mashada ya maua na kuwasha mishumaa.

Akiwa nyumbani kwa Baba wa Taifa pia, kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa alikabidhi pikipiki kwa kikundi cha vijana, kukagua mradi wa kikundi cha wanawake, kufungua kikundi cha wapinga rushwa na kupatiwa maelezo kuhusu Jukwaa la Mobile Kilimo.  

Aidha Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru kitaifa akiwa eneo hilo alitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ujumbe wa Mwenge kitaifa kwa mwaka 2021.

Mwenge wa Uhuru unakesha leo katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyamsisi na kesho unatarajiwa kukabidhiwa katika Wilaya ya Bunda ili kukamilisha mbio zake katika Mkoa wa Mara.

 Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu tarehe 28 Juni 2021 asubuhi kuendelea na mbio zake mkoani humo.   

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.