• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtanda: Uchunguzi wa mauaji Butiama unaendelea

Posted on: May 30th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo ameshiriki msiba wa Mwandu Malegesi mmoja kati ya waendesha pikipiki (bodaboda) wanne waliouawa katika Wilaya ya Butiama na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia tarehe 27 Mei, 2023 na kuwataka wananchi kutulia wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi .

Akizungumza katika msiba huo na katika kijiwe cha bodaboda katika Kitongoji cha Kuoko, Kijiji cha Nyamikoma Wilaya ya Butiama Mhe. Mtanda amewataka wananchi kuwa watulivu na kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi wakati linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

“Tutapambana na jambo hili hadi wanaohusika wakamatwe ili matukio ya namna hii yasijitokeze tena katika Wilaya ya Butiama na Mkoa wa Mara” amesema Mheshimiwa Mtanda.  

Mheshimiwa Mtanda ametoa pole kwa wafiwa wote na kukemea vikali mauaji yaliyotokea katika Wilaya ya Butiama na kuahidi kushirikiana na wananchi kutokomeza vitendo hivyo.

“Mimi nina wajibu kusimamia usalama wenu na wananchi wote wa Mkoa wa Mara ……kama Serikali tunafahamu umuhimu wa usalama katika shughuli za usafirishaji mnazofanya na tunalichukua jambo hili kwa uzito unaostahili lakini tunaomba ushirikiano ili iwe rahisi kuwabaini wahusika” amesema Mhe. Mtanda.

Amewahakikishia waendesha bodaboda kuwa “Mimi pamoja na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara tutafanya uchunguzi wa kina kwa sababu tukio hili ni mara ya tatu sasa linajirudia katika eneo hili” amesema Mhe. Mtanda.

Katika eneo hilo, Mkuu wa Mkoa amepokea kero mbalimbali za wananchi na bodaboda hao na kuzitolea ufafanuzi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.